Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, Serikali ina mipango gani ya kuliendeleza Bonde la Mto Ruvu kwa kushirikiana na wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niombe kufanya marekebisho kidogo kwa sababu Bonde la Wami Ruvu sio Bonde la Mto Ruvu haya ni mabonde mawili tofauti lakini pamoja na marekebisho hayo na majibu mazuri ya Serikali juu ya Bonde la Wami Ruvu naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali haioni sasa ni muda sahihi Wizara ya Maji kushirikiana na Wizara ya Mifugo kwenye Jimbo la Kibaha Vijijini kwenye Kata ya Kwala na Dutumi kujenga mabwawa ili kuzuia mifugo isiende kuharibu kingo za Mto Ruvu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa kuna kazi nzuri imefanywa na Serikali kwenye Bonde la Wami Ruvu la kuunda vikundi na kutambua namna wanavyoweza kutoa huduma kwa wafugaji.

Je, Shughuli hizi ambazo zimefanywa kwenye Bonde la Wami Ruvu Serikali haioni sasa ni muda sahihi kuja kuzifanya kwenye Bonde la Mto Ruvu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Michael Mwakamo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote Mheshimiwa Mbunge nakupongeza kwa uelewa, hili ni Bonde la Wami Ruvu lakini unahitaji zaidi tujikite kwenye Bonde la Ruvu na huku kote Bodi yetu ya Maji ya Wami Ruvu inafanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na ushirikiano na Wizara ya Kilimo nikutoe hofu sisi ni Serikali tunafanya kazi kwa team work kwa hiyo, tutashirikiana na Wizara ya Kilimo kuhakikisha tunaendelea kujenga maeneo ya kunyweshea mifugo maeneo yale kule yenye wafugaji kwa lengo la kuzuia uharibifu kwenye kingo za huu Mto Ruvu na hili tutalifanya kwa umoja wetu kwa kushirikiana kama Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na Jumuiya za watumia maji upande wa Ruvu. Tutahakikisha viongozi ambao wanasimamia Bonde la Wami Ruvu namna walivyofanya upnde huu wamesikia watafanya. Lengo ni kuhakikisha ushirikishwaji wa pamoja unafanyika kwa pande zote.