Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, Mkoa wa Kagera unachangia kiasi gani kwenye Pato la Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mkoa wa Kagera anaosema unachangia 2.6% ni mkoa ambao una rutuba ya kutosha, unazalisha kahawa ya kutosha na pia una ardhi ya kutosha: Je, huo mkoa kuchangia kwenye pato la Taifa 2.6% haioni kwamba ni kushindwa kwa Serikali? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Mkoa wa Kagera umezungukwa na nchi mbalimbali ikiwepo Rwanda, Burundi na maeneo mengine: Nini mkakati wa kuusaidia au kusaidia kuvutia wawekezaji katika huu mkoa ili uweze kuzalisha vya kutosha na hasa katika viwanda ili uongeze pato la Taifa? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anatropia, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali haijashindwa na ushahidi wa hilo, Serikali imeweka mazingira wezeshi ili wananchi wenyewe wafanye shughuli zao za kiuchumi na kijamii.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Serikali imefanya mikakati mbalimbali na hatua mbalimbali. Hivi leo tunaona sekta za uzalishaji ndiyo ambapo Serikali imeweka nguvu zaidi ya kuwekeza mfano kama kilimo cha umwagiliaji, mifugo na uvuvi, ahsante. (Makofi)