Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Je, mpango wa ujenzi wa Reli ya Kusini umefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Mkoa wa Ruvuma umejaliwa kuwa na makaa mengi sana na inasemekana kwamba makaa yaliyopo yanaweza kuchimbwa kwa miaka isiyopungua 80; na sasa Liganga Mchuchuma imefunguka: Je, kwa nini Serikali isitafute mwekezaji kwa mfumo wa BOT (Jenga, Endesha na Kabidhi) kwa base ya makaa ya mawe yaliyopo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa kwa sasa kumekuwa na usafirishaji wa makaa ya mawe kwa malori mengi sana, malori 250 kwa siku na tani 360,000 kwa mwezi na kumekuwa na malalamiko ya wananchi kwamba Mkoa wa Ruvuma na Mtwara tunafaidikaje: Je, Serikali inaweza kuja na taarifa rasmi, yaani tani ngapi mpaka sasa hivi zimeshasafirishwa na Mkoa wa Ruvuma umepata nini; na Taifa linapata nini? (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia suala hili la ujenzi wa reli katika ushoroba huu wa Mtwara. Ni kweli kwamba tayari Serikali tumeshaanza ku-engage ubia kwa maana ya PPP na kuna nchi zaidi ya tano ambazo zimeonesha nia ya kuwekeza, kwa maana ya kuna nchi ya Marekani, Afrika Kusini makampuni kutoka katika hizo nchi, Morocco, Italy, Croatia pamoja na Canada, kwa maana ya kwamba makampuni haya yapo tayari kushirikiana na Serikali katika kujenga reli hii kwa mfumo wa ubia.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusu manufaa na kuja na taarifa rasmi hapa Bungeni, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote wa Mikoa ya Mtwara, Lindi pamoja na Njombe kwamba Serikali ipo tayari kuja na taarifa ya manufaa ya uwepo wa makaa ya mawe katika maeneo hayo tangu tulipoanza kuchimba mpaka sasa. Kwa kupitia pia wenzetu wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara pamoja na Wizara ya Fedha tutashirikiana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee nampongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha, Shilingi bilioni 15 kwa kuanza malipo na fidia kwa maeneo haya la Liganga na Mchuchuma na tayari wameanza kutoa elimu katika maeneo haya. Ni jambo la kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, ahsante sana. (Makofi)