Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA aliuliza:- Je, nini chanzo cha ugonjwa wa manjano kwa watoto wachanga?

Supplementary Question 1

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa kwenye jibu la msingi Waziri ametuambia chanzo ni upungufu wa chembechembe nyekundu kwenye mwili wa mtoto. Sasa je, tunamshauri nini mama mjamzito ili kuondokana na tatizo hili? (Makofi)

Swali langu la pili; mtoto akishazaliwa na akagundulika ana tatizo hili la manjano, wataalam wetu huwashauri wazazi kuwaanika watoto juani. Ni, lini tiba ya ugonjwa huu itapatikana ili kuondokana na changamoto kubwa ya wazazi wanaokumbana na ugonjwa huu wa manjano, baadhi wanapoteza maisha na hatimaye kupunguza nguvu kazi ya Taifa letu? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge. Swali lake la kwanza anasema kwamba tumesema chanzo ni upungufu, siyo upungufu, wakati mwingine watoto wanapokuwa wamezaliwa halafu wanakuwa na chembechembe nyingi za damu ambazo alitoka nazo tumboni zinapokuwa zinasafishwa kunakuwepo sasa na bilirubin ambayo inasababisha hiyo hali ya umanjano kwamba sasa hicho ndiyo kinachotokea. Wakati mwingine kwa sababu ini la mtoto anapozaliwa ndani ya siku 14 anakuwa bado ini lake halijakua vya kutosha, kwa hiyo, uwezo wa kubadilisha ile kitu kinachosabisha umanjano haina uwezo wa kutosha ndiyo maana unaona huo umanjano, kwa hiyo, ni kitu cha kawaida. Ikitokea kama tulivyosema ndani ya masaa 24 basi ni tatizo tunalifuatilia na kujua. Hata hivyo ikitokea baada ya masaa 24 ni muhimu vilevile wataalam kumuangalia.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ni suala la kwamba watoto wanaanikwa juani. Nimuambie tu Mheshimiwa Mbunge, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshafanya revolution kubwa sana, ndiyo maana umeona trilioni 1.3 imefanya mabadiliko makubwa sana ya tiba ya afya. Leo unaona vifaa vingi sana vimesambazwa kwenye maeneo yetu na vituo vyetu vya afya, utaona kuna vifaa maalum vya kuwaweka watoto ambavyo vinatoa mionzi maalum kwa ajili ya kuondoa hilo tatizo. Kwa hiyo, watoto wetu kwa revolution aliyoifanya Dkt. Samia Suluhu Hassan mpaka kwenye vituo vyetu na zahanati sasa vifaatiba vinaenda kununuliwa na hili tatizo litaondoka. (Makofi)

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA aliuliza:- Je, nini chanzo cha ugonjwa wa manjano kwa watoto wachanga?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Ninaomba kuuliza, je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na changamoto ya ugonjwa wa rheumatic heart disease ambao unaonekana unaongezeka kwa kasi kubwa? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kikubwa ambacho naweza kumwambia Mheshimiwa Mbunge moja ni elimu, watu kuangalia afya zao kila wakati na kupata tiba stahiki mapema, ndiyo maana unaona leo, hata Taasisi yetu ya Jakaya Kikwete keshokutwa inakwenda Pemba kwenda kabisa kule vijijini kuhakikisha watu wanafanyiwa uchunguzi na kuhakikisha haya matatizo yanagundulika mapema na watu kupata tiba stahiki mapema. (Makofi)

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA aliuliza:- Je, nini chanzo cha ugonjwa wa manjano kwa watoto wachanga?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa.

Je, Serikali ina mpango gani kusaidia wagonjwa wanaohitaji viungo bandia kama vile miguu bandia, kwani gharama zake ziko juu sana kwa mgonjwa wa kawaida. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, alichokisema Mheshimiwa Ndakidemi ni kweli na kuna tatizo hilo na ndiyo maana bado tulikuwa tunasisitiza, mwarobaini wa tatizo hili la uwezo wa kulipia tiba ni Bima ya Afya kwa wote hilo ndiyo la kwanza. Kumekuwepo na utaratibu wa Serikali kusaida Watanzania wasiojiweza, wale ambao watathibitika hawana uwezo wa kujilipia basi kuna utaratibu unakwenda kwa Mtendaji wako wa Kata anaandika barua na kuna social welfare kwenye hospitali zetu wanazipitia basi anapata exemption anaweza kuhudumiwa. (Makofi)