Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kuhusu hewa ya ukaa ili wananchi waelewe na wanufaike na elimu hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bajeti ya Serikali ya 2023/2024 imepanga kutoza asilimia 10 ya mapato ya mnufaika ambaye ni mkulima; kwa nini Serikali isisamehe tozo hiyo kwa wakulima wadogo ili kuwavutia wakulima hao kwenye kuwekeza zaidi kwenye uvunaji wa carbon?

Swali la pili, Mwongozo wa Carbon wa mwaka 2022 umejikita zaidi katika biashara za carbon za misitu mikubwa, lakini Serikali haimtambui mkulima huyu mdogo; je, Serikali itaboresha lini mwongozo huo ili biashara ya carbon kwa wakulima itambulike rasmi? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuanzia na swali la kwanza; suala la uwepo wa tozo ni suala ambalo lipo kisheria, lakini jambo la kusamehewa tozo ama kupunguza hiyo tozo pia lipo kisheria. Mimi nimwombe tu Mheshimiwa kwamba atupe muda twende tukakae na Wizara inayohusika, wakiwemo wenzetu Wizara ya Fedha, tuone namna ya kuweza kuzungumza nao ili lengo na madhumuni kuweza kuwapa nafasi wakulima wadogo wakaweza ku-invest zaidi kwenye carbon baada ya kupunguziwa tozo hiyo, kwa sababu biashara hii inalenga zaidi kule kwenye community.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira, juhudi ya kwanza ambayo tumeifanya ni kutengeneza kanuni na miongozo, jambo ambalo limeshakamilika. Lakini ni kweli tumeona na tumegundua kwamba kuna baadhi ya mapungufu, na sasa hivi ninavyozungumza tumeshaanza kuzifanyia review kanuni hizi. Hivi ninavyozungumza kuna timu yetu ipo Morogoro imekaa kwa ajili ya kufanya baadhi ya mapendekezo kuongeza vitu ili mradi tuweze kuwapa nafasi wakulima na wengine.

Mheshimiwa Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge baada ya review hii tutaona maboresho makubwa yatakayokuja kugusa kwenye sekta za wakulima, sekta za wafugaji na sekta za wafanyabiashara. Nakushukuru.