Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza kilimo cha minazi?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, kwanza niishukuru Serikali kuwa na mkakati mzuri wa kuboresha kilimo cha nazi nchini. Nitaomba niwe na swali moja tu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Dar es Salaam pembezoni kwa maeneo ya Kibamba, Segerea na Ukonga pamekuwa na vikundi vingi vinafanya kilimo cha mbogamboga; je, ni upi mkakati wa Serikali kuwawezesha hawa ili wafanye kilimo bora cha mboga mboga?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali hivi sasa imeweka mkazo mkubwa kwenye kuhamasisha kilimo cha mboga mboga na matunda ili kuongeza uzalishaji ambao kwa mwaka uliopita kupitia mazao haya yametuletea fedha za kigeni zaidi ya dola milioni 750 na lengo letu kufikia dola bilioni 1.2 kwa mwaka 2030. Hivyo kwa hivi sasa tunaendelea kuwawezesha wakulima wadogo wadogo kwanza kabisa katika upatikanaji wa green houses ambao utasaidia katika uzalishaji mkubwa au vilevile mbegu bora ambayo pia itasaidia katika kuzalisha kwa wingi na sambamba na hilo pia tunatafutia masoko kupitia mwamvuli wa TAHA ambao hivi sasa tumeshafungua masoko mengi na wakulima wengi wameanza kuuza mboga mboga na matunda nje ya nchi kupitia mwamvuli huu wa TAHA.

Kwa hiyo, kama Serikali pia tutahakikisha masoko ya uhakika yanapatikana ili tuendelee kuhamasisha vijana wengi zaidi kushiriki katika kilimo hiki cha mboga mboga.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza kilimo cha minazi?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Katika Wilaya yetu ya Kilwa zao hili la minazi limekuwa likiabiliwa na changamoto ya magonjwa mbalimbali na hivyo kupelekea uzalishaji kushuka na umaskini kuongezeka kwa wazalishaji wa zao hili la minazi.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua changamoto ya magonjwa ya minazi katika Wilaya ya Kilwa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kupitia Kituo cha Utafiti cha Kilimo Mikocheni hivi sasa tunaendelea kufanya utafiti wa kuja na miche bora ambayo itakuwa kinzani ya magonjwa na hasa ugonjwa wa manjano ambao unaathiri sana nazi na kufifisha uzalishaji na kwa hivi sasa tunaendelea na uzalishaji wa mbegu mbili kubwa ya East African Tall pamoja na dwarf ambazo zenyewe zina ukinzani mkubwa wa magonjwa naamini pia wakulima wa Kilwa watanufaika na mbegu hizi na wataongeza uzalishaji kwa sababu kazi ya utafiti imekwisha kufanyika.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza kilimo cha minazi?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kutokana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri amesema ataleta mbegu bora za minazi.

Je, katika uletaji wa mbegu bora za minazi mtaangalia na zile mbegu za asili ambazo zilikuwa ni bora zaidi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu (TPHPA) pale Arusha tunayo benki ya kutunza vinasaba vya mbegu zikiwepo mbegu za asili, kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba tutayazingatia hayo yote pamoja na mbegu za asili ili mwisho wa siku tuhakikishe kwamba uzalishaji unaongezeka, lakini vilevile tunazitunza mbegu zetu hizi kwa sababu zimekuwa zina manufaa makubwa kwa wakulima wetu kwa miaka mingi kabla hatujaleta mbegu hizi ambazo zinatumika hivi sasa.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza kilimo cha minazi?

Supplementary Question 4

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuendeleza kilimo cha michikichi kwenye Mkoa wa Songwe kwa sababu uoto wa eneo hilo unakubali zao hili?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba zao la mchikichi linaendelea kulimwa katika maeneo yote ambako tumepima afya ya udongo na inakubali na kwa Mkoa wa Songwe kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema sasa hivi tuko katika uzalishaji wa miche na wenyewe pia tutauweka katika mpango wa kuhakikisha kwamba wakulima wa Songwe wanapata miche ya michikichi na wanafanya uzalishaji kama katika haya maeneo mengine.