Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami kilometa 2.8 za barabara ambazo ni mchepuko kwenye barabara ya Pipeline?

Supplementary Question 1

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kutoa fedha ambazo zilikwenda kukamilisha ujenzi ule na usimamizi wa Engineer Masige pamoja na Mkuu wa Mkoa barabara ile hatimaye ikakamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru pia kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali ni lini itaanza ujenzi wa barabara kutoka Katumba – Kapugi - Ushirika? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kutoka Kiwira – Isangati kutokea Mbalizi ambao huo ni mpango ulio kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nikianza na barabara ya kwanza bahati nzuri hizi barabara zote nazifahamu mimi binafsi, lakini Barabara ya kwanza ya Katumba – Kapugi hadi Ushirika hii barabara bado ilikuwa haijafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na Meneja wa Mkoa hii ni pamoja na Kiwira na Isangati ameshaanza kuzitembelea hizo barabara ili aweze kubaini gharama za kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara yote ya Katumba – Kapugi - Ushirika lakini pia Ushirika – Isangati - Mbalizi.

Mheshimiwa Spika, baada ya hapo sasa ndiyo Serikali itaanza kufikiria kuijenga kwa kiwango cha lami baada ya kukamilisha usanifu wa kina, ahsante. (Makofi)

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami kilometa 2.8 za barabara ambazo ni mchepuko kwenye barabara ya Pipeline?

Supplementary Question 2

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi; je, ni lini barabara ya kutoka Kimo – Iponjola – Ikuti – Ibungu mpaka Kafwafwa itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantona, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hiyo ni barabara ambayo inaunganisha Mkoa wa Mbeya kwa maana ya Wilaya ya Rungwe na Wilaya ya Ileje na katika mwaka huu wa fedha tunaouendea imetengewa Bajeti kwa ajili ya kuanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kutoka Ibungu – Katengele – Kafwafwa hadi Kimo, ahsante. (Makofi)

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami kilometa 2.8 za barabara ambazo ni mchepuko kwenye barabara ya Pipeline?

Supplementary Question 3

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Mji wa Njombe kwa sababu ya wingi wa malori unahitaji kuwa na bypass. Je, ni lini Serikali itaanza kufanya bypass kutoka Kibena kwenda mpaka Yakobi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tulishatoa maelezo hapa kwamba tuna mambo mawili tutafanya. Moja, kuanzia hapo Kibena tunategemea kujenga barabara za njia nne kwa ajili ya kupunguza msongamano, lakini pia sasa hivi Meneja wa Mkoa kulingana na ukuaji wa Mji wa Njombe wameanza kufanya study ya kuona wapi barabara ya bypass itapita na hasa tukizingatia kwamba Mji wa Njombe umekua, kwa hiyo wanaangalia maeneo ambayo hawataingia gharama kubwa ya kutoa fidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo sasa hivi wako wanatembea, baada ya hapo sasa wataweka hiyo ramani kwenye maandishi kwa ajili ya kuiombea fedha kuanza hiyo kazi ya kutengeneza hiyo bypass, ahsante. (Makofi)

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami kilometa 2.8 za barabara ambazo ni mchepuko kwenye barabara ya Pipeline?

Supplementary Question 4

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, Barabara ya kutoka Iyombwe – Kisanga – Malolo mpaka Kilolo ni barabara ambayo inahudumiwa na TAZAMA lakini ni barabara muhimu sana ya kuunganisha Mkoa wa Morogoro na Iringa.

Je, Serikali ina kauli gani kutumia barabara hii kama mbadala wa barabara kuu ya kutoka Mikumi kwenda Mbeya?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyotaja ni kweli ni muhimu na kwa sasa Serikali inachofanya ni kuhakikisha kwamba inakarabatiwa kwa kiwango cha changarawe wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuifanyia usanifu ikiwa ni maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami kilometa 2.8 za barabara ambazo ni mchepuko kwenye barabara ya Pipeline?

Supplementary Question 5

MHE. ALLY. A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, mwaka 2018 Mheshimiwa Rais aliahidi kujenga Barabara ya kutoka Mbambo – Ntaba – Ipinda; je, Serikali imefikia wapi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Mlaghila, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema kwamba Kiongozi wa Taifa alishaahidi, atakubaliana nami kwamba barabara hii tayari imeshafanyiwa usanifu wa kina na sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)