Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, lini mgogoro wa ardhi wa Shamba la Kambenga utatatuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa msingi wa maamuzi wa Mahakama unatokana na offer iliyotolewa tarehe 2 Julai, 1990 na offer hiyo ilikuwa ni ya miaka 33 mpaka leo tukihesabu ndugu Kambenga hana umiliki tena wa shamba hilo;

(a) Je, Serikali pamoja na nia njema ya mazungumzo yanayoendelea haioni sasa imefika wakati wa kurejesha shamba hilo kwa wananchi?

(b) Je, ni lini Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kuambatana na mimi kwenda kusikiliza wananchi hawa ili asikilize kilio chao? Ahsante.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kunambi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la kuwa na offer ya miaka 33 na offer ikaisha haimnyimi uhalali kama ameomba tena kuendelea kulimiliki, na wakati huo huo kama hakuna mwombaji mwingine ambaye ameomba maana yake lile eneo linaweza likawa liko wazi kwa ajili ya wengine. Mpaka sasa tunavyoongea mwenye shamba hilo bado analitumia kwa hiyo tunaweza kusema kwamba bado anayo haki yake kwa ajili ya kumiliki eneo lile kwa sababu mpaka sasa hakuna mwombaji mwingine yeyote aliyeomba eneo lile.

Mheshimiwa Spika, suala la pili la lini niko tayari kuambatana naye, tutaangalia ratiba kwa sababu tayari tukimaliza Bunge hili tumeshajipangia ratiba ya kuzunguka katika Mikoa, tutaangalia Morogoro iko lini na tutafika kama iko kwenye awamu hii.