Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuvutia Wawekezaji wa Viwanda vya kuchakata Madini ya chumvi Wilayani Kilwa?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, na ahsante sana Serikali kwa kunijibu swali langu vizuri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, napenda kuiuliza Serikali; kwa kuwa biashara ya wazalishaji wetu wa chumvi katika Mkoa wetu wa Lindi imekuwa ikiathiriwa na waagizaji wa chumvi kutoka nje ya nchi.

(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia hawa wafanyabiashara wadogo wadogo waanze kufanya biashara ya chumvi kwa ufanisi?

(b) Je, Serikali sasa haioni wakati umefika wa kuweza kuwa na bei elekezi kwa zao hili la madini ya chumvi kwa Mkoa wetu wa Lindi ili kuhakikisha kwamba hawa wafanyabiashara wa chumvi katika Mkoa wetu wananufaika na biashara hii?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, ni kweli kwamba kumekuwa na changamoto katika sekta hii ya chumvi kwa maana ya baadhi ya viwanda kuagiza malighafi ya chumvi kutoka nje badala ya kuchukua chumvi inayozalishwa hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, tulishatoa maelekezo na hili ni agizo la Serikali, kwamba wenye viwanda wote wanaozalisha chumvi hapa nchini watumie malighafi kwa maana ya chumvi inayozalishwa nchini, kwa hiyo tulishatoa marufuku kuagiza chumvi kutoka nje ya nchi kwa ajili ya viwanda vya ndani.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu bei elekezi, tunashukuru kwa sababu tunadhani biashara zinatakiwa ziende kwa uhuru, kwa maana ya supply and demand, lakini pale inapotokea hoja mahsusi muhimu kama hii tutangalia ikiwa kuna ulazima wa kuweka bei elekezi kwa ajili ya kuona wananchi wa Tanzania, na hasa wanaozalisha chumvi ghafi, waweze kupata bei nzuri inayouzwa kwenye viwanda vya Tanzania, nakushukuru sana.