Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutokomeza kabisa ugonjwa wa Malaria nchini?

Supplementary Question 1

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mkoa wa Kagera una maambukizi makubwa ya Malaria, ni namba tatu kwa maambukizi makubwa Kitaifa na kwa kuwa Wilaya ya Ngara ndiyo inayoongoza katika maambukizi ya Malaria Mkoani Kagera. Je, ni lini sasa Serikali itatusaidia kufanya unyunyiziaji wa viuatilifu (Indoor Residual Spraying) katika Wilaya ya Ngara ili kupunguza maambukizi ya Malaria?

Swali la pili, kwa kuwa zipo nchi duniani ambazo tayari zimeshatokomeza kabisa Malaria. Je, ni lini Tanzania tumelenga ni mwaka gani tutakuwa tumefikia zero Malaria, kwa maana ya kutokomeza kabisa Malaria? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ni kuhusu Mkoa wa Kagera. Ni kweli kwamba Mkoa wa Kagera ni Mkoa wa tatu una asilimia 18 ukiongozwa na Tabora wenye asilimia 23 ukifuata Mtwara. Ni kweli Ngara inaongoza na tulikwenda na tunao ushirikiano na wenzetu wa Rwanda katika kutokomeza na tumeshajenga vituo upande wa Tanzania na upande wa Ngara kwa ajili ya kuweka utaratibu.

Mheshimiwa Spika, moja ni huu ambao amesema kunyunyuzia hiyo dawa, lakini tunafikiria kwa sababu Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati anazindua Malaria Council alielekeza kwamba tuandike Wizara ya Fedha tuoneshe tunahitaji shilingi ngapi kwa ajili ya kununua zile dawa za kuua viluilui na tayari tumeshafanya na tumewasilisha Wizara ya Fedha bilioni 22 kwa ajili ya nchi nzima na mojawapo Ngara kwa maana ya Mkoa wa Kagera ikiwepo ni sehemu ya kufanya kazi hiyo.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu ni lini tutaweza kutokomeza Malaria. Kwanza nikuhakikishie kabisa kuna Mikoa zaidi ya tisa sasa ni chini ya asilimia moja Malaria kwenye nchi yetu, na Mikoa mingi sana imeshuka. Kwa hiyo, tunadhani mpaka 202030 nchi yetu nayo itafikia kwenye kiwango cha hizo nchi nyingine. (Makofi)