Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka Gari la Wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Mlola Wilayani Lushoto?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pia nishukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali ni lini itapeleka fedha kujenga Vituo vya Afya katika Kata ya Kwayi pamoja na Kata ya Makanya? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Kituo cha Afya Gare kimezungukwa na kata mbili ambazo hazina vituo vya afya. Je, Serikali haioni sasa ipo haja ya kupeleka gari la wagonjwa ili kurahisha huduma kwa wananchi wetu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shekilindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, la kwanza hili kuhusu ujenzi wa Vituo vya Afya vya Kwayi na Makanya, tutakaa na Mheshimiwa Shekilindi kuona katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya Ujenzi wa Vituo vya Afya katika Halmashauri yao na tuhakikishe fedha hizi zinakwenda katika walau kituo cha afya kimojawapo, kwa sababu ni mpango wa Serikali wa kujenga vituo vya afya kwenye maeneo ya kimkakati nchini kote ikiwemo Kwayi na Makanya.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la gari ya wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Gare. Mheshimiwa Mbunge ni shahidi kwamba muda siyo mrefu kituo hiki cha afya kimetoka kukamilika kwa maana kilipelekewa fedha na tayari kimeshakamilika. Sasa kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imenunua magari 316 kwa ajili ya kila Halmashauri kupata walau magari mawili ya wagonjwa. Sasa magari haya mawili yatayoelekea kule Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto waelekeze moja katika Kituo hiki cha Afya cha Gare. (Makofi)

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka Gari la Wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Mlola Wilayani Lushoto?

Supplementary Question 2

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa magari ya wagonjwa yaliyoagizwa na Serikali yanakuja kwa awamu, je, Serikali haioni umuhimu kwa awamu ya kwanza kuanza na Hospitali ya Mji Handeni kwa sababu haina gari la wagonjwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, magari haya yanakuja kwa awamu kama ambovyo nimesema awali na kila Halmashauri ilikuwa tumepanga kupeleka magari mawili na gari lingine la tatu kwa ajili ya monitoring and evaluation katika Halmashauri hizi.

Mheshimiwa Spika, tunapokea ushauri ambao umeutoa wa kuangalia Halmashauri zile ambazo zitakuwa zina eneo dogo lakini lile gari la monitoring and evaluation, bado litakwenda kwa ajili ya kuhakikisha kwamba huduma za afya zinasimamiwa vizuri.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali la Mheshimiwa Kwagilwa, tutakaa naye na kuona katika awamu hii ya kwanza, Hospitali ya Mji pale Handeni inaweza kupata gari pia. (Makofi)