Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kutatua changamoto ya upatikanaji wa mbolea nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsnate. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali langu la kwanza, mmesema Serikali imejipanga kuipa kampuni yetu ya TFC mtaji wa bilioni 40 na sasa hivi tumebakiwa na miezi mitatu tu tufike kwenye high season ya kuhitaji mbolea. Je, mtatumia muujiza gani kuhakikisha mmeagiza mbolea na mnaisambaza nchi nzima?

Swali langu la pili, ni kwa nini CPB hawataki kuwarudishia wakulima fedha, walizoahidi kuwapa mahindi wakati Serikali imezuia CPB isitoe mahindi, na fedha zao hamtaki kuwarudishia ni kwa nini na mnarudisha lini hizo fedha?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nilitoa taarifa humu ndani Bungeni na naomba leo nirudie ya kwamba Serikali imejipanga kuhakikisha ifikapo mwezi wa saba mbolea zote za kupandia na kukuzia ziwe zinapatikana kwa wakulima ili waanze msimu na mbolea zikiwemo.

Mheshimiwa Spika, nakata nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba TFC walianza maandalizi haya mapema na hivi sasa tuko katika hatua za mwisho kuanza kupokea shehena za meli ambazo tutashusha mzigo huo, pia tunayo mbolea ya kutosha kuanzia kwa wakulima katika msimu unaoanza hivi karibuni. Kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba jambo hilo litafanyika.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, nimesikia hoja yake ya CPB na wakulima, naomba nikae na Mheshimiwa Mbunge nipate hayo madai ya wakulima, mimi na CPB tutakaa tuone namna ya kuweza kutatua jambo hili, ili mwisho wa siku tuweze kuhakikisha kwamba wakulima wanapata haki yao.