Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, upi mpango wa kuwapa mafunzo Majukwaa ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi ngazi za Vitongoji, Vijiji, Kata na Wilaya – Pwani?

Supplementary Question 1

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza naishukuru sana Serikali kutupongeza Mkoa wa Pwani kwa kufanya vizuri, lakini pia kwa kutenga kiasi cha shilingi milioni 161 kwa kuanza hayo mafunzo. Maswali yangu mawili ya nyongeza ni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, je, ni lini hasa mafunzo hayo yataanza kwa kuwa majukwaa yale yameundwa muda mrefu na tumefanya jitihada mpaka Kitongoji, Vijiji, Wilaya mpaka na Mkoa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa katika jibu lake la msingi amesema zimetengwa hizo fedha shilingi milioni 161 na ndani yake kutakuwa na za Mkoa wa Pwani, lakini nataka niulize, je, Serikali inaipa wajibu gani Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupitia Katibu Tawala wa Mkoa na Halmashauri zetu za Mkoa wa Pwani katika kulea majukwaa haya ili yalete tija iliyokusudiwa? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, swali lake la kwanza kama nilivyoeleza kwenye jibu la msingi, Serikali imetenga shilingi milioni 161 kwa ajili ya kuwajengea uwezo na kuwajengea uwezo wanawake ili kuinuka kiuchumi ambapo Mkoa wa Pwani umetengewa shilingi milioni 58.5 kwa ajili ya kuendesha mafunzo hayo.

Niwaombe tu Maafisa Tawala wa Mikoa wote nchini waanze kuandaa programu hizo za mafunzo na mwaka wa fedha ukiingia mafunzo hayo yaanze. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, zipo taasisi mbalimbali za binafsi ambazo zinawezesha wananchi kutoa mikopo mmoja-mmoja na vikundi. Kwa hiyo, niwaombe wananchi waendelee kutumia fursa hizo kuhakikisha uchumi wao unakua, ahsante. (Makofi)

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, upi mpango wa kuwapa mafunzo Majukwaa ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi ngazi za Vitongoji, Vijiji, Kata na Wilaya – Pwani?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ziko baadhi ya Halmashauri hapa nchini ambazo mapato yake sio toshelevu hivyo hawawezi kutosheleza kutoa mikopo ya asilimia 10.

Je, ni upi mkakati wa Wizara hii kuwawezesha wanawake kiuchumi kuanzia ngazi ya kitongoji na vijiji?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inawaagiza Maafisa Tawala wa Mikoa na Maafisa Ustawi wa Jamii waendelee kutoa elimu kuhakikisha wananchi wote wanapata elimu, ili kuweza kujiinua kiuchumi na kuhakikisha wanakuwa vizuri katika maisha yao na maendeleo yao. (Makofi)

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, upi mpango wa kuwapa mafunzo Majukwaa ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi ngazi za Vitongoji, Vijiji, Kata na Wilaya – Pwani?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa watu wengi hawafahamu uwepo wa Sheria ya Manunuzi ya asilimia 30 kwa makundi maalum. Sasa je, Serikali ina mkakati gani kueneza uelewa juu ya uwepo wa sheria hii ya asilimia 30 ya manunuzi kwa makundi maalum ambayo ni wanawake, vijana na watu wenye ulemavu? Ahsante.

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Spika, labda kwa kuwa linakwenda kwenye sekta zote ninaomba tu niseme kwamba kwa sababu Serikali inafahamu umuhimu wa makundi hayo tutajipanga ndani ya Serikali ili sekta zote zihakikishe zinasimamia jambo hili na makundi hayo maalum ambayo yamekwisha kutamkwa kwenye sheria hiyo waweze kunufaika. Hiyo ni fursa muhimu sana kwa maendeleo na ustawi wa Taifa. (Makofi)