Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha matengenezo ya miundombinu ya usambazaji maji katika kata sita za Muheza?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIS M. MWINJUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na nashukuru kwa majibu mazuri na ya kutia moyo ya Serikali hasa kuhusiana na bomba la kilomita 14.5 na tarehe yake ya kukamilika. Hili ni moja ya matatizo tu nataka kupata commitment ya Serikali kuhusiana na tarehe ya kukamilika kwa mfumo mzima wa usambazaji ukiachilia mbali kilomita 14.5? Hilo ni la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kama muda utaruhusu naomba kuambatana na aidha Waziri au Mheshimiwa Naibu Waziri kwenda Muheza ili jibu atakalonipa kwenye swali langu la nyongeza akawape wananchi wa Muheza pamoja na kujionea mwenyewe jinsi miundombinu ya usambazaji wa maji Wilayani Muheza kwenye Kata hizi za Mbaramo, Genge, Masuguru, Tanganyika, Majengo na Kwemkabala vilivyokuwa hoi, ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hamis Mohamed Mwinjuma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kukupongeza sana Mheshimiwa Mbunge jitihada zako za kuweza kushirikiana na Wizara zinafahamika, commitment ya Wizara ni kuhakikisha muda ambao usanifu unataka mradi kukamilika tutajitahidi kufanya hivyo hizi kilomita 14.5 kuhakikisha zinakamilika na maji yatoke bombani, wananchi waweze kufurahia fedha ambayo Mheshimiwa Rais ametaka iwafikie. Lengo ni kuwatua akina Mama ndoo kichwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuambatana ni moja ya taratibu zote mara baada ya Vikao vya Bunge aidha mimi ama Waziri ukinihitaji mimi hakuna neno tutakwenda tukafanye kazi. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha matengenezo ya miundombinu ya usambazaji maji katika kata sita za Muheza?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa, katika Mji wa Ilula uliyoko katika Wilaya ya Kilolo unao mradi ambao umeshakamilika kwa muda mrefu lakini changamoto kubwa ni usambazaji wa maji katika vitongoji vyote.

Je, lini Serikali au katika bajeti hii itatoa pesa ili maji yaweze kusambazwa katika Mji wa Ilula? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kabati kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe ni shahidi Mheshimiwa Kabati ni mfuatiliaji mzuri sana wa miradi ya maji kukamilika. Suala la mradi ambao tayari umekamilika usambazaji unafuata hiyo ndiyo hasa Wizara inashughulika nayo. Sisi tunapenda kusema mradi umekamilika pale maji yanapotoka bombani mwananchi ananufaika. Hivyo kwa mradi kama huu ambao umekamilika usambazaji ndiyo hatua inayofuata kwa mwaka ujao wa fedha.