Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kurahisisha huduma ya upatikanaji wa bima ya afya kwa wananchi wake?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, Mheshimiwa Mariam Kisangi ana maswali mawili ya nyongeza.

Swali lake la kwanza linasema; ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam kumekuwa kuna ucheleweshwaji wa upatikanaji wa kadi za bima za afya yaani toka tarehe mtu analipia mpaka kuja kuipata ile kadi inaweza kuchukua hata miezi sita. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba kadi hizi zinapatikana kwa wakati? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili; linasema kumekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wa figo wagonjwa ambao wanahitaji huduma ya kuzisafisha hizi. Nini kauli ya Serikali kuruhusu wagonjwa hawa kuwa na Bima za Afya hata kama ni zile za vifurushi vikubwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, labda nijibu maswali yake mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja; ni ucheleweshaji wa bima ya afya ukilipia; ni ukweli kwamba umewekwa utaratibu kwamba toka unapolipia basi upate bima yako baada ya miezi mitatu na lengo lilikuwa ni moja tu kwamba watu wengi wakiwa na afya, wakiwa salama, wanakuwa hawana tabia ya kujiunga na bima watu wakadhani kwamba ni vizuri mtu akajiunga wakati hana ugonjwa wowote ili kulinda mfuko huo.

Lakini hili la miezi sita kwakweli nilakushughulikia kwamba tulishughulikie mapema ili watu wapate ndani ya muda uliopo. Lakini sasa wakati muswada unakuja hapa ambao sisi Wabunge ndiyo tutakaojadili basi tujadili tuone tunatakiwa upate kwa wakati gani na tutaweka utaratibu mzuri ambao hautaleta matatizo ambayo sasa mnayaona.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu wenzetu wenye matatizo ya figo; moja ni kwamba sisi wote tushirikiane kwa sababu suala moja ni kuhakikisha kwamba watu hawafiki mahali wanapata matatizo hayo ya figo, lakini ikitokea sasa wamepata basi kwa kweli Serikali inajitahidi.

Moja; ilikuwa kufanya dialysis kwa mara moja ni shilingi 380,000 lakini sasa hivi imeshuka mpaka shilingi 120,000 lakini bado ni gharama kubwa. Tutaendelea kuona namna ya kufanya ili hao watu wapungukiwe na mzigo kwa sababu kwanza wengi hawana uwezo wa kufanyakazi na wengine hawana kazi. (Makofi)