Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea Wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mkalama?

Supplementary Question 1

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kwanza kabisa kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Singida Vijijini, inakabiliwa na ukosefu wa gari la kubebea wagonjwa. Je, ni lini Serikali itapeleka gari katika hospitali hii ili kuokoa vifo vya kinamama wajawazito na watoto?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa kituo cha afya cha Sepuka, kiko pembezoni na hakina gari la kubebea wagonjwa. Je, ni lini Serikali itapeleka gari katika kituo hiki cha afya?

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru.(Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aysharose Ndogholi Mattembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kwali kwamba ni kweli kwamba Hospitali ya Halmashauri ya Singida Vijijini inahitaji gari la wagonjwa na Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi wote katika Halmashauri zetu kote nchini itapeleka magari ya wagonjwa ndani ya mwaka huu wa fedha au mapema mwaka ujao wa fedha ikiwemo Halmashauri ya hii ya Singida Vijijini.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Kituo cha Afya cha Sepuka ambacho kiko pembezoni, tumefanya tathmini ya kuona vituo ambavyo viko pembezoni ambavyo vinahitaji magari ya wagonjwa vitapelekewa magari ya wagonjwa.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mheshimiwa Aysharose Ndogholi Mattembe, amekuwa akifuatilia sana masuala ya maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa Singida na Watanzania kwa ujumla nimhakikishie kwamba tutaendelea kumpa ushirikiano. (Makofi)

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea Wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mkalama?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Nataka nimuulize swali Naibu Waziri, kuna Halmashauri zingine zina Majimbo zaidi ya mawili au matatu, sasa kama mtapeleka gari moja, hilo gari litaenda kwenye Jimbo gani? Kwa nini usiweke wazi, kwa nini isiwe kwa Majimbo badala ya kuwa Halmashauri? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Mwenisongole, Mbunge wa Jimbo la Mbozi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mpango wa kupeleka magari ya wagonjwa kwenye Halmashauri unazingatia vigezo, kigezo cha kwanza ni idadi ni ya watu katika Halmashauri, kigezo cha pili ni idadi ya wagonjwa kwa maana ya burden of disease katika Halmashauri husika. Utaratibu huu hauzingatii Majimbo kwa sababu Majimbo pia yanatofautiana na idadi ya wananchi ukilinganisha na Halmashauri. Kwa hiyo, tutakwenda kupeleka magari haya, kwa kigezo cha Halmashauri na idadi ya watu na burden of disease. Pale ambapo itahitajika kwa Majimbo mawili kupata gari tutafanya hivyo. (Makofi)