Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, ni aina gani ya madini yanapatikana ndani ya Wilaya ya Kalambo kulingana na tafiti ambazo zimekwishafanywa na Serikali? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini.

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili kama ifuatavyo:-
(a) Mpaka sasa Wizara imeweza kutoa leseni ngapi za utafiti wa madini katika Wilaya ya Kalambo?
(b) Kwa kuwa kuna taarifa kwamba kuna uwezekano mkubwa sana wa kupatikana mafuta hasa ndani ya Ziwa Tanganyika ambalo linafika mpaka Kalambo, je, Serikali imefanya jitihada gani za makusudi kuhakikisha kwamba utafiti huu unafanyika na kukamilika ili tuweze kupata mafuta ndani ya Ziwa Tanganyika na Ziwa Rukwa kwa ujumla wake?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu leseni ngapi tumetoa, eneo la Kalambo bado linafanyiwa utafiti mkubwa sana na Wakala wa Jiolojia. Mpaka sasa leseni ambazo zimeshatolewa katika eneo la Kalambo ni tano tu ambapo leseni tatu za uchimbaji ambazo zimetolewa kwa Kampuni ya Agricultural Fast Limited na leseni mbili zimetolewa kwa kampuni ya binafsi ambayo inaitwa Shamze Ahmed Limited ambazo ni za madini ya dhahabu. Hata hivyo, bado eneo hili linafanyiwa utafiti na hadi sasa kuna waombaji wengine wameomba leseni nne za uchimbaji ambao ni pamoja na Mheshimiwa Antony Chilumba ambaye ameomba leseni za utafutaji wa madini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la utafutaji wa mafuta, ni kweli kabisa eneo la Ziwa Victoria, Ziwa Natron, Eyasi na mengine mpaka Wembere bado TPDC na makampuni mengine wanafanya utafiti. Kwa eneo la Ziwa Tanganyika bado hawajagundua mafuta pamoja na gesi kwa ajili ya kufanyiwa utafiti wa kina. Bado TPDC na makampuni mengine wanafanya utafiti na wako katika hatua nzuri za kuweza kubainisha kama mafuta yanapatikana au la. Namuomba Mheshimiwa Mbunge avute subira, TPDC wanaendelea na ukaguzi ili kuona kama bado kuna mafuta maeneo ya Ziwa Tanganyika.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, ni aina gani ya madini yanapatikana ndani ya Wilaya ya Kalambo kulingana na tafiti ambazo zimekwishafanywa na Serikali? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini.

Supplementary Question 2

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa mujibu wa taarifa ya Waziri wa Fedha, moja ya sababu ambazo zinasababisha shilingi yetu kushuka ni matumizi makubwa ya fedha za kigeni na katika bidhaa ambazo zinaagizwa ni makaa ya mawe. Ni kwa nini makaa ya mawe ya Tanzania hayatumiki tunaagiza makaa ya mawe kutoka South Africa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza anataka kujua kwa nini makaa ya mawe yaagizwe kutoka nje badala ya kutumika ya hapa nchini? Ni kweli kabisa, sasa hivi makaa ya mawe yanayopatikana yangeweza kupatikana kwa wingi sana pale Kiwira kwenye eneo la Kiwira lenyewe, lakini hata Kabulo. Kiwira ni kweli kabisa, kutokana na utafiti wa mwaka 2007 iko reserve ya tani milioni 30 na pale Kabulo ni tani milioni 50 lakini bado kuna maeneo mengi ya Mchuchuma na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ilizochukuwa Serikali sasa ni kuhakikisha kwamba wawekezaji wote wanapata makaa ya mawe kwa sababu yanajitosheleza. Hata hivyo, wako wawekezaji kama Dangote alikuwa anaagiza kutoka Afrika Kusini na maeneo mengine sasa hivi tumesitisha kutoa vibali vya kumruhusu kuingiza isipokuwa tunamlazimisha aanze kutumia makaa ya mawe ya hapa. Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kusema Serikali itaanza sasa kuchukua hatua kuhakikisha makaa ya mawe yatakayopatikana hapa yananunuliwa hapahapa nchini.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, ni aina gani ya madini yanapatikana ndani ya Wilaya ya Kalambo kulingana na tafiti ambazo zimekwishafanywa na Serikali? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini.

Supplementary Question 3

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Kumekuwa na taarifa zilizotapakaa katika mitandao ya kijamii zinazoeleza ugunduzi wa gesi aina ya helium. Je, Serikali inaweza kutueleza nini juu ya taarifa hizo, ni za kweli au ni za uongo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ni kwamba, utafiti umefanywa na vyuo ambavyo vinatambulika duniani kimojawapo ni Oxford na Durham na wamepiga mahesabu kutokana na utafiti wa Jiofizikia uliofanywa miaka ya 80 na 90 wakafikia kiwango cha gesi ya helium.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna tofauti hapa ya hizi gesi, helium inapatikana kwenye kina kifupi lakini hii gesi nyingine methane inapatikana kwenye kina kirefu na duniani ambaye ana helium nyingi ni Marekani. Kwa hiyo, gesi kule Marekani inaanza kupungua ndiyo maana na sisi tunaitafuta kwa udi na uvumba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilichogundulika ni kutokana na mahesabu ya huko nyuma na kinachofuata kwa miezi michache inayokuja Helium One ikishirikiana na watalaam wengine watafanya drilling ya huko Ziwa Rukwa. Hapo ni upande wa Ziwa Rukwa ndiyo imepatikana kiasi hicho estimate ya kwanza 54.2 billion metric cubic feet. Hata hivyo, watachimba kule Lake Rukwa, wataenda Eyasi, wataenda Natron nadhani baada ya kama mwaka mmoja hivi tutajua kwamba tunaweza kuanza kuuza helium duniani. Kwa hiyo, hizo ni taarifa za uhakika zinatoka chuo cha uhakika cha Oxford.

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, ni aina gani ya madini yanapatikana ndani ya Wilaya ya Kalambo kulingana na tafiti ambazo zimekwishafanywa na Serikali? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini.

Supplementary Question 4

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu utafutaji wa madini katika eneo la Kalambo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, sasa hivi kule mitaani kuna malalamiko kwamba utafutaji umepungua sana, wawekezaji hawaji kwa sababu ambazo hazielezeki. Kwa nini Serikali sasa isichukue hatua madhubuti ili kuhakikisha kwamba utafutaji unakua na tuweze kupata migodi mingine siku za usoni? Ahsante sana.

Name

Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Answer

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, msemaji ni geologist nilikuwa nadhani anajua jiolojia na madini duniani yanakwendaje. Hayo yaliyoko mitaani sio ya kitaalam kwamba utafiti umepungua. Ni kwamba kila baada ya miaka fulani madini yanatafutwa yanawekwa store yanakuwa mengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya vita ya kwanza, Wajerumani na Wafaransa walileta vijana wao kutafuta madini Afrika. Kufika mwaka wa sitini, madini yakawa ni mengi sana duniani ndiyo maana utafutaji ulizorota hata sekta yetu ya madini miaka ya 70, 80 ikazorota. Miaka ya 90, madini yakapungua dunia, utafutaji ukawa wa nguvu sana na Afrika ilichukuwa asilimia 30 ya bajeti ya utafutaji wa madini duniani kote.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimuambie Mheshimiwa Mbunge kwamba, hata China ambayo ndiyo mchimbaji na mtumiaji mkubwa wa chuma duniani vilevile amepunguza kutumia chuma na ndiyo maana unaona hata Zambia uchumi wao umeyumba kwa sababu walikuwa wanategemea sana shaba iliyokuwa inapelekwa China. Kwa hiyo, hili sio jambo la Tanzania ni kwamba dunia ina madini mengi, utumiaji wa chuma,shaba umepungua sio kwa Tanzania tu lakini utafutaji utakuja tena, hilo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, teknolojia ya dunia inabadilika huwezi ukang‟ang‟ania kila siku dhahabu, chuma au shaba. Sasa hivi madini yanayotafutwa kwa wingi sana duniani ni haya nilivyosema yanayotumika kwenye simu zetu, rare earth elements. Madini hayo hayajapungua duniani yanatumika kwenye simu, televisheni, kwa hiyo, yanatafutwa kwa nguvu sana.
Kingine ambacho kinatafutwa madini ya kutengeneza mabetri kwa sababu hesabu inaonyesha kwamba itakapofika karibu mwaka 2040, asilimia kubwa ya magari mengi duniani yatakuwa ni yanayotumia umeme. Kwa hiyo, madini kama graphite na mengine ndio yanatafutwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, siyo kwamba utafutaji umepungua bali ni madini gani utafutaji wake umepungua. Sababu ni teknolojia ya dunia inabadilika na sisi Tanzania tunajielekeza kwenye madini ambayo ni adimu na ambayo yanatakiwa duniani. Ahsante.