Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza napenda kushukuru Serikali yangu sikivu kwa jitihada zake inazozifanya kuibua miradi ya vituo vya Polisi nchini.

Mheshimiwa Spika, kituo cha Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, kilianza kujengwa toka mwaka 2016, hadi hii leo 2022 kituo hicho bado hakijamalizwa. Kilijengwa kikapigwa plasta baadhi ya vyumba, chooni bado, nje hakijapigwa plasta hadi hii leo Polisi wapo Wilaya ya Kati wameazimwa eneo la vitambulisho ndiko wanakofanyia kazi zao. Je, Serikali itamaliza lini Kituo hiki cha Polisi cha Dunga, ili Polisi waweze kufanya kazi kama kawaida?(Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake makini juu ya kituo hiki na juhudi zilizofanywa na wananchi katika kujenga kituo hiki mpaka hatua iliyofikiwa, ulituelekeza siku moja hapa na mimi nikajibu kwamba Wizara inaandaa mpango wa kumalizia vituo na kujenga maeneo ambayo hayana vituo kabisa. Kipaumbele kitawekwa kwenye maeneo ambayo tayari wameshajenga vituo kama hawa wa Dunga. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika mwaka ujao tutafanya kila liwezekanalo ili ukamilishaji wa kituo hicho uweze kuanza.

Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana.(Makofi)

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, wananchi wa Jimbo la Ushetu wamejichanga wakafanikiwa kujenga msingi wa Kituo cha Polisi lakini mpaka leo ni zaidi ya miaka mitatu Serikali haijafanya chochote. Sasa, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi kwa wananchi wa Jimbo la Ushetu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cherehani kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunafahamu Ushetu ni moja ya Wilaya mpya ambazo hazijawa na Vituo vya Polisi ngazi ya Wilaya na kwenye Kata mbalimbali. Pia tunatambua juhudi ambazo zimefanywa na wananchi kuanza ujenzi wa vituo hivi na Serikali inao wajibu wa kusaidia kukamilisha. Ninapenda kumuahidi Mheshimiwa Mbunge kama nilivyokwishasema kwenye jibu la msingi kwamba kipaumbele kitawekwa kwenye maeneo ambayo wananchi na wadau wameanza kujenga vituo hivyo ili kuvisaidia ujenzi huo uweze kukamilika. Nashukuru.

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 3

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Wilaya ya Butiama haina Kituo cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ghati Chomete, Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Mara kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Wilaya ya Butiama ni moja ya Wilaya mpya ambazo hazina Vituo vya Polisi ngazi ya Wilaya na Kata zake mbalimbali hazina vituo hivyo. Kama nilivyokwishasema kwenye jibu langu la msingi, kipaumbele katika ujenzi wa Vituo vya Polisi utazingatia Mikoa, Wilaya na Kata ambazo hazina kabisa vituo lakini msisitizo utawekwa kwa wale ambao tayari wana maeneo na wameanza kujitolea. Kwa hiyo, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba Wilaya ya Butiama ni moja ya eneo litakalozingatiwa katika bajeti ijayo. (Makofi)

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 4

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali moja la nyongeza lakini nami niwapongeze Yanga kwa kupata Ubingwa baada ya kusota kwa miaka minne ndiyo leo wanapumua hapa unawasikia, ubingwa ulikuwa mikononi mwa Simba. Baada ya kuwapongeza naomba niulize swali moja la nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Waziri, utakubali kuongozana nami kufika Mvumi kujionea hali ilivyo kwa askari wa pale Mvumi Misheni ili tuweze kujenga kituo pamoja? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lusinde kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hakuna shida kabisa, baada ya Bunge hili tutazingatia ratiba ili tuweze kuongozana tukatizame changamoto zinazowakabili wananchi wa Kata zako ambako hakuna Vituo vya Polisi ili tuweze kushirikiana kuvikamilisha. Nashukuru sana.

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 5

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, vitendo vya uhalifu vimekithiri sana katika Kata ya Berege iliyopo Jimbo ya Mpwapwa. Je, Serikali itajenga lini Kituo cha Polisi ili kukabiliana na wimbi hili la uhalifu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Malima, Mbunge wa Mpwapwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba baadhi ya maeneo hasa Miji inayokua na kuchipua ikiwemo Wilaya ya Mpwapwa kuna kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu. Kama nilivyowahi kusema hapa, uhalifu ni zao la jamii lakini si jambo jema kufanywa na vijana wetu ambao wanazo fursa mbalimbali wakizitumia wanaweza kupata riziki zao bila kulazimika kuleta uhalifu katika jamii. Kwa hiyo, nichukue nafasi hii kulitaka Jeshi la Polisi ngazi ya Mikoa, Wilaya na Kata kuimarisha shughuli za usimamizi wa usalama wa raia na mali zao lakini kuchukua hatua thabiti dhidi ya vijana au watu wanaojihusisha na matendo ya uhalifu. Nashukuru sana.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 6

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii yakuuliza swali la nyongeza. Wananchi wa Jimbo la Kishapu, wadau wa maendeleo pamoja na Mfuko wa Jimbo tumechangia zaidi ya Milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya. Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuambatana na mimi kwenda kuona jitihada za wananchi na kuweka mchango wa Serikali?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Butondo, Mbunge wa Kishapu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nakubali kuongozana na Mheshimiwa Butondo ili kwanza kutambua juhudi zilizofanywa na wananchi, wadau pamoja na yeye mwenyewe kupitia Mfuko wake wa Jimbo. Pili ni kuona namna ambavyo Serikali inaweza kuchangia kukamilisha kituo hiki cha ngazi ya Wilaya. Nashukuru sana.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 7

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi. Ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande Kata ya Chamazi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdallah Chaurembo Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza tunatambua juhudi za Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Jimbo lake Mbagala kwa juhudi wanazofanya katika kuimarisha usalama wa raia na mali zao. Kwa kutambua juhudi hizo, nasi kama Serikali kupitia Jeshi la Polisi tutatembelea Kituo cha Mbande kutathmini kiasi gani kinahitajika ili kuweza kumalizia na hivyo kutoa mchango wetu ili kukamilisha kituo hicho kama sehemu ya kuunga mkono juhudi za wananchi.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 8

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Kituo cha Polisi cha Sumbawanga Mjini Mkoani Rukwa ni cha toka enzi za mkoloni, ni kidogo hakina hewa. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunatambua wilaya za zamani ikiwemo Wilaya ya Sumbawanga ina Vituo vya Polisi ambavyo moja vimejengwa muda mrefu baadhi vimeanza kuwa chakavu lakini vingine havikidhi haja ya viwango vya Vituo vya Polisi vinavyotakiwa kuwepo sasa hivi ngazi ya Wilaya. Kwa hiyo, ninachukua dhima kumuahidi Mbunge kwamba katika kazi tunayoifanya ya kuimarisha maeneo ambayo hayana kabisa vituo, jambo jingine ni kukarabati na kuboresha vituo vya kizamani ili kuweza kukidhi mahitaji ya sasa. Kwa hiyo, Sumbawanga itakuwa ni eneo litakalozingatiwa.

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 9

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Tuangoma ni Kata yenye mkusanyiko wa watu wengi sana na kata hiyo haina Kituo cha Polisi. Je, ni lini Mambo ya Ndani mtajenga Kituo cha Polisi pale Kata ya Tuangoma?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Janejelly Ntate Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Dar es Salaam kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Tuangoma ni moja ya Kata za Jiji la Dar es Salaam ambao haina Kituo cha Polisi, nimuombe Mheshimiwa Mbunge na especially Mbunge wa Jimbo achangie kidogo na kuhamasisha wadau kushiriki ili Serikali ije isaidiane nanyi kukamilisha, kama ambavyo maeneo mengine wamefanyakazi hiyo. Nashukuru sana.

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 10

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, Jimbo la Buchosa lina takriban idadi ya watu wasiopungua 400,000 lakini na kituo cha Polisi katika Mji Mdogo wa Nyehunge ambacho hadhi yake ni ndogo sana. Je, ni lini Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kutembelea kituo hiki ili aweze kukiona na hatimaye kufikia maamuzi ya kujenga kituo kingine?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Eric Shigongo Mbunge wa Buchosha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni bahati njema kwamba nimepanga kufanya ziara katika Mkoa wa Mwanza na Wilaya hii ni sehemu ya Mkoa wa Mwanza. namuahidi Mheshimiwa Mbunge, nitakapofanya ziara eneo hilo nitatembelea eneo ya Nyehunge ili kuona ni nini tushirikiane na Mbunge kufanya kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi kama njia ya kuimarisha usalama wa raia kwenye maeneo hayo. Ahsante sana.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 11

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kauli yake kwamba Serikali itaunga mkono jitihada za wananchi. Pale Mzinga Injinia Cyprian Romeja na wananchi wenzake wamechanga Milioni 108 na Mbunge amechangia Milioni 8.7 kwa ujenzi wa Kituo cha Polisi. Je, ni lini Serikali itakamilisha Kituo kile cha Polisi kwa kutuchangia fedha za ujenzi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa Mbunge wa Ukonga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nafahamu juhudi za Mheshimiwa Silaa na mara kadhaa amenishirikisha juhudi wanazozifanya ikiwemo kuchangia ujenzi wa vituo hivi, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika mpango wetu wa uboreshaji, ukamilishaji na uendelezaji wa Vituo vya Polisi eneo la Mzinga ni moja ya Kata itakayozingatiwa katika ukamilishaji huo. Nashukuru sana.

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 12

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Wananchi wa Kiharata katika Kata ya Mapinga wamepambana wamepata kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi. Je, Serikali ipo tayari kutusaidia ili tuweze kukamilisha Kituo hicho mapema?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shabani Mbunge wa Bagamoyo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunafahamu juhudi za Mbunge na wananchi wa Jimbo lake katika kutunza usalama raia na mali zao na uwepo wa Vituo vya Polisi ni moja ya mahitaji ya kukamilisha jambo hilo. Ninamuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutashirikiana nae mwenyewe, wadau wa Wilaya ya Bagamoyo pamoja na wananchi ili kujenga kwenye kiwanja hiki cha Mapinga ambacho wananchi wamejitolea kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho. Ni moja ya eneo tutakaloingia kwenye mipango yetu ya uendelezaji wa Vituo vya Polisi. Nashukuru.

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Supplementary Question 13

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami ningependa nimuulize swali moja dogo la nyongeza Mheshimiwa Waziri. Je, Jimbo langu la Chumbuni tumekuwa na matatizo sana ya hivi vituo na tumekuwa hatuna kituo zaidi ya mwaka wa nne, tumekuwa tukisema sana lakini tumekuwa tukiahidiwa na Wizara kuwa itakuja kushughulikia. Mheshimiwa Waziri upo tayari nasi tukijenge kile kituo kwa nguvu zetu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ussi Pondeza Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, natambua juhudi za Mheshimiwa Mbunge, wamefanya mambo mengi katika Jimbo lake ikiwemo kuanza ujenzi wa vituo hivi, nilitembelea huko na nikaona. Ninamuahidi katika maeneo tutakayozingatia na kuyapa kipaumbele katika utekelezaji wa mpango wetu wa ukamilishaji na ujenzi wa vituo, Jimbo la Chumbuni litapewa kipaumbele. Nashukuru sana. (Makofi)