Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 1

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kuambatana na mimi ili ukaweze kunidhibitishia mradi huu utakamilika mwaka huu wa fedha? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kutokana na changamoto nyingi wanawake wanazozipitia kipindi wanachokuwa wajawazito; Je, Serikali haioni haja kushusha huduma hii Wilayani ili tuweze kupata huduma hii kwa Mkoa wa Shinyanga kwa Watoto Njiti? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Santiel Erick Kirumba Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja niko tayari kuandamana naye kwenda Shinyanga na nitafurahi tukiwa wawili tu peke yetu. Ahsante. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni kwamba Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kupeleka kwenye hospitali za Wilaya huduma hizi. Kwenye bajeti yetu Mheshimiwa Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alisema kwamba, kwa mwaka huu unaokuja wa fedha tunaenda kujenga sehemu za Watoto Njiti 100 na siyo tu kwenye hospitali za Wilaya na kwenye Vituo vya Afya. Kwa hiyo, fedha zimeshapatikana sasa imebaki kuwasiliana na Waziri wa TAMISEMI ili kupanga sehemu za vipaumbele vya kuanza na kwa jiografia ya Mkoa wa Shinyanga ni mojawapo ya maeneo yataenda kufaidika na huu ujenzi. Ahsante sana.

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Hospitali ya Mkoa ya Tumbwi siyo kwamba inahudumia watu wa Pwani tu na wale wapita njia. Kitengo cha Watoto Njiti kweli kipo lakini uboreshaji ni pamoja na vifaa tiba. Watoto wanazaliwa pale lakini inabidi wakimbizwe.

Je, ni lini Serikali pamoja na kuboresha kitengo cha Watoto Njiti na vifaa tiba vitaboreshwa lini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dokta Kaijage kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwamba Hospitali ya Tumbwi ni mojawapo kweli kuna eneo la Watoto Njiti lakini hospitali inazidiwa. Katika Bilioni 59.3 ambazo zimetengwa kwa ajili ya uboreshaji, Hospitali ya Mkoa wa Tumbi ipo mojawapo na eneo ambalo limetengewa hela kwa ajili ya kulipanua na kuongezea vitanda ni eneo hilo la Watoto Njiti. (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 3

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, Serikali haioni haja ya kumjumuisha mtoto njiti kwenye Bima ya Mama yake ili pindi anapozaliwa aweze kupata huduma hiyo na kumwondolea Mama mwenye mtoto njiti adha ya kuanza kufanya usajili wa mtoto kwenye Bima ya Afya?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, swali aliloliuliza Mbunge ni swali muhimu sana na nitumie fursa hii kumwagiza Mkurugenzi Mkuu wa Bima ya Afya kwamba suala la kuhudumia mtoto njiti ambaye mama yake ana bima yake ya afya lisiwe mjadala. Mtoto njiti akizaliwa na huduma yake inakuwa ni automatic. Vilevile kwa sababu tunakwenda kwenye suala la bima ya afya kwa watu wote Wabunge wote tukumbuke hayo mambo tuhakikishe sasa tutaweka kwenye sheria ijayo iweze kufanyika vizuri zaidi. (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 4

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Katika Hospitali yetu ya Mkoa wa Iringa tuna kitengo cha Watoto Njiti na tuna upungufu mkubwa wa mashine na dawa inaitwa Lung surfactant ambayo dozi moja inauzwa Shilingi Laki Tano na mtoto ili a-survive anahitaji dozi tatu. Serikali ina mpango gani kuangalia kwamba dawa hizi angalau zinawekewa ruzuku ili kupunguza gharama hiyo? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, moja kwanza sioy dawa kuwekewa ruzuku kwa taratibu na sheria na taratibu za Wizara ya Afya ni kwamba huduma ya mtoto chini ya miaka Mitano including hawo Watoto Njiti na Mama na Mtoto ni bure. Kwa maana kwamba tunaposema mlitupitishia bilioni 200 kwa ajili ya kununua dawa na vifaatiba. Hilo eneo tutakwenda kulielekeza nguvu nyingi kuhakikisha kwamba Watoto njiti hawawezi kukutana na matatizo hayo.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 5

MHE. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, Hospitali ya Kahama inahudumia watu kutoka pembezoni kwa maana ya Mikoa ya Tabora pamoja na Geita. Je, ni lini Serikali itaboresha kituo cha Watoto njiti pale Hospitali ya Kahama?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nijibu swali la Mheshimiwa hapa, ukisikia Serikali inasema inajenga vituo vya afya kwa kila Tarafa na kazi ile imeendelea kufanyika kupitia TAMISEMI ni kwenda kupunguza wagonjwa ambao sasa wanaenda kurundikana kwenye hospitali moja kama ilivyo Kahama.

Mheshimiwa Spika, mimi nafikiri Mbunge ni muhimu tukatembelea hospitali hiyo inawezekana tukikaa mle ndani tutaona tu maeneo ambayo tunaweza tukaweka sehemu ya Watoto njiti, ibaki kazi ya kuleta vifaa na kuvipachika na Watoto waweze kupata huduma.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 6

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Serikali imetueleza kwamba wana mpango wa kujenga vituo 100 vya Watoto Njiti hapa nchini; Je, sisi ni miongoni mwa watu tutakaofaidika Jimbo letu la Mchinga kwa kituo hicho?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wao ni wafaidika na Wilaya yake ni sehemu ambayo inafaidika, kuna utaratibu ambao unatumika hata ndani ya miezi miwili ijayo kuna vifaa vinapelekwa kwenye Jimbo lake kwa ajili ya huduma ya Watoto Njiti.

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 7

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Ni dhahiri kwamba viko visababishi ambavyo vinapelekea mama kujifungua mtoto njiti ikiwemo mahitaji ya lishe. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba inaimarisha huduma za lishe kwa akina mama wajawazito ili waweze kufikisha full term yaani mtoto azaliwe ndani ya umri anaotakiwa kuzaliwa? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu ameshaelekeza, kumekuwepo na makongamano mengi, kumekuwepo na semina nyingi ambazo zinazungumzia suala zima la lishe. Sasa badala ya kufanya makongamano na semina fedha hizo zitaelekezwa kununua vitamini ambazo zina multiple vitamin na akina mama wajawazito wote wanapewa hizo vitamin. Lakini niendelee kuwaomba Wabunge wa kike na wa kiume mojawapo ya sababu za Watoto Njiti ni stress. Sisi wote tunapofika mahali kina mama wajawazito wanakuwepo tuhakikishe mazingira yao ya kufanya kazi lakini sisi wanaume tuwe karibu nao ili kuondokana na mambo mengine yanayoweza kuzuilika yanayosababisha uwepo wa Watoto Njiti.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Swali langu nilikaa nikafikiri kwamba ultrasound machine pamoja na x-rays ni muhimu sana kwenye suala zima la Watoto Njiti. Kwa hiyo nilitaka nimuulize Waziri kwamba ni lini watepeleka ultrasound machine na x-ray katika kituo cha Afya Himo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, labda nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mimi na yeye nikimaliza haya maswali kama kituo chake hakina ultrasound tukae chini ili tuweze kuelekeza MSD wapeleke mara moja ultrasound kwenye eneo lake. Pia suala la x-ray kuna fedha zile ambazo Waziri wa Afya amesema zimeokolewa tumefanikiwa vilevile kupata x-ray 33 za ziada, kwa hiyo katika hiyo ziada tutaona tunaelekeza maeneo gani baada ya watalaam kuchakata na kuona vipaumbele.(Makofi)

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 9

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Tunayo changamoto kubwa sana katika Hospitali ya Rufaa ya Kitete iliyopo Mkoani Tabora ya chumba ama kitengo maalum kwa ajili ya Watoto Njiti. Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha kitengo hiki ili kuweza kukidhi mahitaji yaliyopo hivi sasa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Katika hospitali ambazo zimetengewa fedha kwa mwaka huu wa fedha Bilioni 59.3 mojawapo ni hospitali ya Kitete. Kwa maana hiyo eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge unalisema tutaenda kulingalia kwa umakini zaidi. Pia maeneo ya kutembelea inawezekana tatizo siyo sehemu ya kuweka Watoto Njiti lakini maamuzi katika kupanga vyumba inawezekana tunahitaji tu vifaa. Tutaenda kuangalia kwa pamoja Mheshimiwa Mbunge halafu tuone tunafanya nini kama ni uhitaji wa vifaa tutaweka vifaa mapema. (Makofi)

Name

Bakar Hamad Bakar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 10

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa ni ahadi ya CCM ya kuimarisha ushirikiano baina ya Wizara hizi ambazo siyo za Muungano. Je, Wizara ya Afya inashirikianaje na Wizara ya Afya ya Zanzibar kwenye kutatua changamoto hizi za Watoto Njiti? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, anachokisema Mbunge ni kweli na nimejaribu kutembelea baadhi ya maeneo upande wa Taifa letu upande wa Visiwani ni kweli kunahitajika maboresho makubwa sana kwenye huduma za afya. Jana Mheshimiwa Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alikuwa anajadiliana na baadhi ya wadau ili kuona ni namna gani hawa wadau ambao wanatoa huduma huku upande wa Bara waweze kwenda upande wa pili wa visiwani na kuweza kuboresha miundombinu ya afya badala ya kupeleka fedha kwenye maeneo hayo. Tayari AMREF wamekubali kuelekea upande huo wa pili kwa ajili ya kuboresha maeneo unayosema Mheshimiwa Mbunge.

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 11

MHE. KABULA E. SHITOBELO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mkoa wa Mwanza una hospitali na vituo ambavyo bado havijapata huduma hii ya chumba cha mtoto njiti.

Je, Serikali lini itakamilisha kutuwekea vyumba maalum kwa mtoto njiti?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni kweli anavyosema lakini kwenye hospitali ya Sekou-Toure ya Mkoa wa Mwanza ujenzi mkubwa sana unaendelea, suala ni kwenda kuamua na kuweka vifaa kwenye eneo hilo ili watoto waweze kupata huduma. Nafikiri anazungumzia Mkoa mzima kwa ujumla na hasa maeneo ya visiwani. Kwa mfano, Ukerewe ambako ni Visiwani sasa hospitali ya Wilaya ile inaenda kujengwa kwa level ya hospitali ya Mkoa ili mambo yote ya Rufaa ya Mkoa yaweze kutolewa huko huko Visiwani. Kwa hiyo, tutaendelea kufanya ziara na kugundua matatizo mbalimbali kwenye maeneo na kuelekeza fedha kadri ya mahitaji ya maeneo husika. (Makofi)