Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 32 Water and Irrigation Wizara ya Maji 279 2022-05-27

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali italishughulikia tatizo la maji kwa vijiji zaidi ya 14 vya Tarafa ya Mtae?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, na kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Tarafa ya Mtae ina jumla ya vijiji 20 ambapo vijiji 16 vinapata huduma ya maji kupitia visima vifupi na mito. Katika kuboresha huduma hiyo, kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imekamilisha ujenzi na ukarabati wa miradi ya maji ya Bokoboko, Shaghayu na Rangwi inayonufaisha vijiji sita vya Masereka, Mamboleo, Kwemtindi, Tema, Mpondekaya na Kweshindo.