Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali italishughulikia tatizo la maji kwa vijiji zaidi ya 14 vya Tarafa ya Mtae?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Serikali nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, Mradi wa Rangwi ambao ameutaja hapa ambao una vijiji karibia vinne vya Goka, Nhelei, Kalumele na Mamboleo ni mradi ambao sasa umechakaa, lakini pia eneo la usambazaji limekuwa dogo kwa sababu idadi ya watu imeongezeka. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuboresha mradi huo?

Pili, katika kata ya Sunga, Tarafa hiyo hiyo ya Mtae vijiji vyote vinne havijawahi kuwa na mradi wowote wa mfumo wa maji ya bomba. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka na kata hii ya Sunga iweze kupatiwa miundombinu ya maji safi ya bomba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shangazi kama ifuatavyo;-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunafahamu mradi ule umechakaa na kama Wizara tayari tumeuweka kwenye mpango wa mwaka 2022/2023 ili kuona kwamba tunakwenda kukarabati na kuweza kuwafikishia wananchi wote wa maeneo aliyoyataja maji mengi, safi, salama na ya kutosha.

Swali lake la pili anaulizia kuhusu Kata ya Sunga ambayo ina vijiji vinne ni kweli mtambao wa mabomba kwenye kata hii haukuweza kufikiwa kulingana na jiografia ya eneo lenyewe. Vyanzo ni kweli viko vingi katika eneo lile, lakini vyanzo vingi viko maeneo ya chini na wananchi vijiji viko kwenye miinuko kwa maana kwenye milima hivi kidogo kama tunavyofahamu jiografia ya Lushoto lakini kama Wizara tunaendelea kuona uwezekano wa kupata vyanzo vya kujitosheleza maeneo yale ya juu na hatimaye kabla ya mwaka ujao wa fedha tutahakikisha tunapata na kuweza kuwafikishia maji ya bombani wananchi wote wa Kata ya Sunga yenye vijiji vinne.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali italishughulikia tatizo la maji kwa vijiji zaidi ya 14 vya Tarafa ya Mtae?

Supplementary Question 2

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru naomba niulize swali moja dogo la nyongeza.

Mji wa Kasera ambayo ndiyo Makao Makuu ya Wilaya ya Mkinga bwawa lake linalopeleka maji hapo linakaribia kukauka, tumeleta maombi ya dharura takriban shilingi milioni 51. Je, ni lini fedha hizi zitapatikana?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kitandula, Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo. Tunatarajia wiki ijayo kuwapelekea shilingi milioni 51 kwa ajili ya bwawa hilo. (Makofi)

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali italishughulikia tatizo la maji kwa vijiji zaidi ya 14 vya Tarafa ya Mtae?

Supplementary Question 3

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Jimbo la Kibiti kata ya Mtawanya kuna vijiji vya Bumba, Msola na Makima vina shida kubwa sana ya maji. Ni nini tamko la Serikali kuhusiana na kuweka maji katika maeneo hayo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Twaha kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kata hii anayoiongelea tumeshazungumza mara kadhaa na Mheshimiwa Mbunge na tayari tunaiweka kwenye utaratibu wa kuona kwamba tunawaletea wananchi maji bombani yakiwa safi na salama.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali italishughulikia tatizo la maji kwa vijiji zaidi ya 14 vya Tarafa ya Mtae?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, ningependa kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri mradi wa miji 24 ni mradi ambao ulikuwa ni mkombozi sana kwenye Mji wa Geita ambapo Jimbo la Geita Vijijini kata tano zilikuwa zinafaidika Senga, Kagu, Nyawilimilwa, Bugurura na Kakubiro. Lakini tumekuwa tukiahidiwa kila siku hatuoni mwelekeo; je, ni lini Serikali itaanza sasa kutekeleza mradi huo wa miji 24?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Musukuma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa NaibU Spika, kwanza niseme siyo vijiji mini 24 bali ni miji 28, lakini vile vile Geita Mjini kata hizo tatu zinakwenda kunufaika hivi punde subira yavuta heri. Maandalizi yote yamekamilika tunasubiri tu kusaini, tunasubiri na muda na nafasi ya Mheshimiwa Rais.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali italishughulikia tatizo la maji kwa vijiji zaidi ya 14 vya Tarafa ya Mtae?

Supplementary Question 5

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaboresha usambazaji wa mabomba ya maji katika Kata ya Bariadi, Mtaa wa Kidinda, Majengo Viwandani?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, usambazaji wa maji katika mji wa Bariadi kwenye maeneo aliyoyataja ni moja ya maeneo ambayo tumeyapa jicho la kipekee kuhakikisha tunakwenda kuyafikia lengo ni kumtua mwanamama ndoo kichwani na kusambaza maji safi na salama.