Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 32 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 281 2022-05-27

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la abiria katika uwanja wa ndege Mtwara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, Mbunge wa Mtwara Mjini, kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Naibu Spika, jengo la abiria katika kiwanja cha ndege cha Mtwara litajengwa katika awamu ya pili ya ukarabati na upanuzi wa kiwanja hicho. Hivyo, fedha itatolewa baada ya kukamilika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya Mradi huu, ahsante.