Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la abiria katika uwanja wa ndege Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa uwanja wa Mtwara inawezekana tukauita international airport kwa sasa package yake ya mradi ule ulikuwa ni kuwepo na gari ya zimamoto nikimaanisha fire. Je, ni lini sasa Wizara itahakikisha kwamba mkandarasi anatuletea gari ya zimamoto pale airport?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili uwanja wa airport umepakana na maeneo ya wananchi, lakini baadhi ya maeneo ya wananchi lilipita bomba la gesi na wananchi wale wakalipwa. Sasa ni lini Serikali itaamua kuwalipa wananchi ambao bado hawajalipwa ili waondokane na adha hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, Mbunge wa Mtwara Mjini kama ifuatavyo:-

Naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika ukarabati na upanuzi wa uwanja huu suala la gari la zimamoto ni sehemu ya mradi huu na tayari mkandarasi ameshatoa order gari itanunuliwa kutoka Ujerumani na thamani yake itakuwa ni bilioni 1.4. Kwa hiyo tayari gari limeshaanza kutengenezwa kwa ajilli ya uwanja wa Mtwara, ahsante.