Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 32 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 282 2022-05-27

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Morogoro – Malinyi – Namtumbo kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutafuata fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Ifakara – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo - Londo hadi Lumecha (Namtumbo) kwa kiwango cha lami. Kwa sasa maeneo yote korofi yataainishwa na kujengwa ili barabara hii ipitike mwaka wote, ahsante.