Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Morogoro – Malinyi – Namtumbo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. NORAH W. MZERU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante ni upi sasa mkakati wa Serikali wa kujenga barabara zote za Morogoro ili ziweze kupitika msimu mzima?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE). Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba baabara zote za Mkoa wa Morogoro zinapitika ni pamoja na kuzijenga zile ambazo tumeziainisha kwa kiwango cha lami, lakini pia kuzitengea fedha barabara zote kwa ajili ya ukarabati na kuna barabara ambazo tayari zipo kwenye kutangazwa kwa ajili ya kuzijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba azma ya Serikali ni kuhakikisha barabara zote zinapitika mwaka mzima, ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Morogoro – Malinyi – Namtumbo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia ametangaza kwa nguvu kubwa utalii kupitia Royal Tour na kwa kuwa barabara zinazokwenda katika Mbuga za Wanyama kama Ruaha National Park hadi leo hazijajengwa kwa kiwango cha lami.

Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba barabara zote zinazokwenda katika mbuga za wanyama zinajengwa kwa kiwango cha lami ili watalii watakapokuja tutendewe haki na Nyanda za Juu Kusini tupate watalii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwa kuanza na barabara ya Iringa kwenda Ruaha National Park, Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara hiyo, lakini pia Benki ya Dunia (World Bank) imeonesha nia ya kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa maana ya barabara zote zinazoenda kwenye mbuga kama ukipitia kwenye kitabu chetu cha bajeti barabara nyingi zinazokwenda kwenye mbuga zimefikiriwa na kutengewa fedha ili kuboresha sekta hii ya utalii ambayo Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan tumeona jinsi ambavyo amefanya kwenye Royal Tour kwa hiyo na sisi hatutamwangusha kuhakikisha kwamba tunatengeneza miundombinu bora kwa ajili ya watalii kwenda kwenye mbunga za wanyama, ahsante.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Morogoro – Malinyi – Namtumbo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kuuliza ni lini barabara ya Kolandoto kwenda Mwangongo yenye kilometa 63 itaanza utekelezaji kwasababu mwaka huu wa fedha imetengewa bajeti ya fedha shilingi 2,000,000,000? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Butondo, Mbunge wa Kishapu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii tumeiweka kwenye mpango kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango la lami kuanzia Kolandoto hadi Lalago na Lalago hadi Mwanuzi kilometa hizi 62 na kilometa 60 katika mwaka huu wa fedha, ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Morogoro – Malinyi – Namtumbo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, hii barabara ya kutokea Namtumbo kwa maana ya Lumecha, Kitanda, Londo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Lupilo wakati Mheshimiwa Waziri anajibu hoja za Wabunge kwenye hotuba yake alisema imeingizwa au imeorodheshwa katika mpango wa EPC, something like that ambao utahusisha wajenzi binafsi.

Mheshimiwa Naibu Waziri unaweza ukawaeleza vizuri wananchi wa maeneo hayo hususani wananchi wa Namtumbo na Malinyi kwa sababu hawakuelewa vizuri mpango huu ukoje ili wajue barabara hii itajengwa na mpango huu lini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye jibu langu la msingi kwanza tutakuwa na mpango wa muda mfupi kuhakikisha kwamba tunaainisha maeneo muhimu korofi tuweze kuyakarabati ili barabara hii ipitike kwa muda wote, lakini kwa suala la EPC+F kwa maana ya Engineering Procurement Construction and Financing, ni suala ambalo litahitaji muda. Nitamuomba Mheshimiwa Vita Kawawa kama ataweza akatuletea swali la msingi ama tutakutana naye ili kuweza kulielezea kwa mapana na marefu kwa ajili ya kutoa uelewa kwa Waheshimiwa Wabunge wote, ahsante.