Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 284 2022-05-30

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:-

Je kwa nini Serikali haitengi fedha za TARURA kwa kuzingatia jiografia, ukubwa wa eneo na mazingira ya Wilaya au Jimbo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA ZA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Jimbo la Same Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, TARURA inaendelea na zoezi la uandaaji wa formula itakayotumika kwenye ugawaji wa rasilimali fedha zinazohitajika kwenye ujenzi na matengenezo na miundombinu ya barabara kulingana na mahitaji ya eneo husika. Formula itazingatia ukubwa wa mtandao wa barabara (road network), thamani ya miundombinu ya barabara iliyopo (asset value), hali ya barabara (road condition), wingi wa magari (traffic volume), idadi ya wakazi (population), mazingira (geographical terrain), kiwango cha mvua (annual rainfall) na kilimo (agriculture potential).