Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je kwa nini Serikali haitengi fedha za TARURA kwa kuzingatia jiografia, ukubwa wa eneo na mazingira ya Wilaya au Jimbo?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Napenda kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa mfano jimbo lake lile la Tunduma, linaingia mara sita kwa jimbo langu, lakini wote tunapata fedha sawa za mgao wa barabara, sasa haoni kama hiyo siyo sawa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Mwenisongole, Mbunge wa Jimbo la Mbozi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli ukichukulia Jimbo la Mbozi, ukifananisha na Jimbo la Tunduma, Jimbo la Mbozi ni kubwa zaidi kuliko Jimbo la Tunduma na utaratibu ambao ulikuwa unatumika mwaka uliopita ni utaratibu ambao tulikubaliana wote Wabunge humu ndani na ndiyo maana sasa hivi tunarekebisho hiyo formula ili majimbo yote yapate kulingana na ukubwa wa eneo na mahitaji ya eneo husika. Ahsante sana.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je kwa nini Serikali haitengi fedha za TARURA kwa kuzingatia jiografia, ukubwa wa eneo na mazingira ya Wilaya au Jimbo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, pamoja na Serikali kutoa pesa nyingi kwa ajili ya miradi ya barabara hizi zinazosimamiwa na TARURA, bado miradi mingi kwenye maeneo imesimama au inasuasua ikiwemo Jimbo la Ukerewe kwa sababu wakandarasi ama kutokuwa na uwezo au kuwa na mrundikano wa kazi nyingi.

Nini kauli ya Serikali juu ya hali hii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Mkundi, Mbunge wa Jimbo la Ukerewe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kauli ya Serikali katika maeneo yote ambayo wakandarasi hawafanyi vizuri ni kuhakikisha kwamba wanamaliza ndani ya muda kwa sababu tumetoa muda kamili wa kufanya ile kazi.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, kama kuna maeneo ambayo wakandarasi wamekuwa hawatekelezi kabisa wajibu wake tunaomba maeneo hayo mtuletee sisi ofisi ya Rais - TAMISEMI kupitia TARURA, ili tuweze kuchukua hatua zikiwemo kuvunja mikataba kwa sababu wanachelewesha hizo kazi. Ahsante sana.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je kwa nini Serikali haitengi fedha za TARURA kwa kuzingatia jiografia, ukubwa wa eneo na mazingira ya Wilaya au Jimbo?

Supplementary Question 3

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi, kauli ya Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati anaongea na Mameneja wa TARURA nchini, alisema kuna mikoa kama Njomba na Mbeya ambayo hali ya barabara ni mbaya lakini ni mikoa ya uzalishaji, TARURA lazima muwape kipaumbele kuwapa fedha; kwa mfano Makete, hali ya barabara ni mbaya.

Ni lini mtaongeza fedha kwa ajili ya mikoa hii ya uzalishaji katika Taifa letu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kuonesha kwamba Serikali inazingatia maeneo yenye uzalishaji mkubwa ndiyo maana utaona katika hizo nyanda ambazo Mheshimiwa Mbunge ameziainisha kuna miradi maalum ikiwemo miradi ya RISE ambayo haiko maeneo mengine, lakini iko katika maeneo ambayo yanazalisha. Tumepeleka huko ili kuongeza fedha nyingi kwa ajili ya uzalishaji katika maeneo hayo. Kwa hiyo, hilo ndiyo jibu sahihi, sio tu fedha za TARURA, ni pamoja na miradi husika. Ahsante sana.