Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 285 2022-05-30

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Maafisa Masuuli na Wahasibu katika Halmashauri wanapata mafunzo juu ya uandaaji wa taarifa za fedha za mwisho za halmashauri?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetoa mafunzo kwa jumla ya watumishi 210 juu ya uandaaji wa taarifa za fedha za mwaka unaoishia tarehe 30 Juni, 2022. Mafunzo hayo yametolewa kwa watumishi waliopo ngazi ya mikoa na halmashauri zote nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha Mwongozo wa Uhasibu katika Mamlaka za Serikali za Mitaa wa mwaka 2020 (Local Authority Accounting Manual) na Waraka wa Ufungaji Hesabu kila mwaka. Maboresho hayo yanakusudia kuzikumbusha taasisi za umma juu ya mambo ya msingi ya kuzingatia na kuwaongoza Maafisa Masuuli na Wahasibu katika kutekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja na uandaaji wa hesabu za mwisho.