Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Maafisa Masuuli na Wahasibu katika Halmashauri wanapata mafunzo juu ya uandaaji wa taarifa za fedha za mwisho za halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, nauliza maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kutokana na uelewa wangu halmashauri zote zilizo nchini zinatofautiana mapato na Serikali imekuwa ikitangaza tu mafunzo ili halmashauri zijihudumie; je, hamuoni sasa kuna umuhimu wa Serikali kupeleka fedha kwa uwiano sawia?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kumekuwa na mfululizo wa hati chafu ambazo ni zaidi ya miaka kumi mfululizo; je, Serikali haioni kwamba inaendelea kupoteza fedha za wananchi kwa kutokuwa na watu wenye weledi au ufanisi mkubwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja ya lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba tunaongeza fedha kwa ajili ya mafunzo na tutazigawa kulingana na uwiano katika halmashauri moja na nyingine, kwa hiyo, hilo ndiyo lengo la Serikali, lengo letu ni kuhakikisha kwamba tunazuia wizi kwa kuwapa mafunzo ya kuweza kuzuia vitendo hivyo vya kihalifu katika halmashauri zetu.

Mheshimiwa Spika, lakini suala la pili kuhusu hati chafu katika maeneo mengi nchini, moja ya kazi kubwa ambayo tumeifanya sasa hivi ni kuhakikisha moja tunawaondoa watu wote wanaosimamia fedha katika maeneo hayo wakiwemo wahasibu, ma-DT pamoja na wakurugenzi. Kwa hiyo, hizo ni hatua ambazo tunachukua, lakini sasa hivi tutakkuwa tunaleta watu ambao ni waadilifu katika maeneo yetu na hatutakuwa tunahamisha kama ambavyo ilikuwa awali mtu anafanya tukio baya upande mmoja tunahamisha katika halmashauri nyingine. Ahsante sana.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Maafisa Masuuli na Wahasibu katika Halmashauri wanapata mafunzo juu ya uandaaji wa taarifa za fedha za mwisho za halmashauri?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; kwa kuwa katika halmashauri kwanza Serikali imetoa mafunzo kwa maafisa 210 ambao ni wachache sana ukilinganisha na halmashauri zilizopo hapa nchini mikoa iliyopo; na kwa kuwa uandaaji wa hesabu unahitaji ujuzi na maarifa maalum ambayo yanatakiwa yatolewe na wafanyakazi wengi wamekuwa hawana maarifa hayo.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba Wahasibu pamoja na Wakaguzi wa Ndani wanapatiwa mafunzo wanayostahili katika utayarishaji wa hesabu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Japhet Hasunga, Mbunge wa Jimbo la Vwawa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana tumejibu hawa tumetoa mafunzo kwa maafisa 210 sasa hivi tumeongeza fedha katika bajeti yetu, kuhakikisha tunawafikia watu wote wa vitengo, wahasibu pamoja na wakaguzi wa ndani ili kuhakikisha kwamba sasa wanafanya kazi ambayo imekusudiwa. Kwa hiyo, fedha zimeongezeka na mwakani tutafanya hivyo kwa watu wote wa idara hiyo.

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Maafisa Masuuli na Wahasibu katika Halmashauri wanapata mafunzo juu ya uandaaji wa taarifa za fedha za mwisho za halmashauri?

Supplementary Question 3

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sheria za uandaaji wa hesabu zimekuwa zimekubadilika mara kwa mara kulingana na mahitaji ya kimataifa; je, sasa Serikali haioni ni wakati sahihi sasa wa kutenga fungu rasmi kwa ajili ya hawa wahasibu ili wakaweze kuhudhuria classes za NBAA?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Simon Songe, Mbunge wa Jimbo la Busega kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali tutaendelea kutenga fedha kadri inavyopatikana lakini kwa sasa tutaendelea na mafunzo ili kuhakikisha kwamba haya yanayotokea sasa hayaendelei. Ahsante sana.