Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 33 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 289 2022-05-30

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:-

Je, kuna mipango gani ya kuweka mazingira wezeshi ya kupata mbegu bora za malisho kama Luseni pamoja na kuwezesha uzalishaji wa mitamba?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuimarisha mashamba yake ya kuzalisha mbegu za malisho kwa kuyapatia vitendea kazi na kuongeza ukubwa wa maeneo ya kuzalisha mbegu za malisho na malisho. Aidha, nitumie fursa hii kuendelea kuihamasisha sekta binafsi kuwekeza katika uzalishaji wa mbegu za malisho na malisho kibiashara ili kukidhi mahitaji ya ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha uzalishaji wa mitamba, mpango wa Serikali ni kuendelea kuyaimarisha mashamba yake ya kuzalisha mitamba ya kituo cha kuzalisha mbegu za mifugo kwa ajili ya uhimilishaji cha NAIC- Arusha ili kuzalisha na kusambaza mitamba na mbegu bora za ng’ombe kwa gharama nafuu.