Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:- Je, kuna mipango gani ya kuweka mazingira wezeshi ya kupata mbegu bora za malisho kama Luseni pamoja na kuwezesha uzalishaji wa mitamba?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nashukuru kwa majibu haya mazuri; lakini kwa kuwa Serikali imeelemewa sana na jambo hili, ina mpango gani sasa au ina vivutio gani kwa sekta binafsi kuzalisha mbegu hizo za malisho pamoja na kuzalisha madume bora ya mbegu? (Makofi)

Swali la pili kwa kuwa kuna uhitaji mkubwa sana wa mitamba bora, mbuzi mapacha, pamoja na vifaranga vya kuku vilivyoboreshwa kwa wanawake wa Mkoa wa Kilimanjaro ambao wanasubiri kwa muda mrefu hata wakati wa kampeni walimuomba Waziri Mkuu alipokuja kufungua kampeni ya Mkoa wa Kilimanjaro. Serikali iko tayari sasa kutoa vitu hivyo kwa ruzuku kwa wanawake hao?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, la kwanza ni juu ya vivutio tulivyoviweka; Serikali imejipanga mara baada ya kupokea maoni ya wadau juu ya kuweza kuweka vivutio kwenye upande wa uzalishaji wa mbegu za malisho, lakini na upande wa uzalishaji wa ng’ombe bora kwa maana ya madume ya mbegu kwa kuondoa baadhi ya tozo.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa ng’ombe bora Serikali imeondoa tozo ya import ya ng’ombe wanaotoka nje ya nchi tulikuwa tukilipisha shilingi 10,000 kwa ajili ya ng’ombe kumkagua na sasa Wizara imependekeza kuondolewa kwa tozo hii na bado tupo katika mazungumzo ndani ya Serikali ya tozo kwa upande wa mbegu za kutoka nje za malisho ili kusudi na zenyewe ikiwezekana ziweze kuondolewa ile tozo na wawekezaji waweze kuweza kufanya kazi hii kwa ufasaha.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni juu ya jambo linalohusu Mkoa wa Kilimanjaro na akinamama kupata ng’ombe wa ruzuku. Katika mwaka huu wa fedha 2022/2023 Serikali imejipanga kuyaimarisha mashamba ya uzalishaji wa ng’ombe bora na ili tuweze kuwasambaza kwa wafugaji kote nchini. Nina imani kuwa akinamama wa Mkoa wa Kilimanjaro watakuwa ni miongoni mwa wanufaika, ahsante sana.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:- Je, kuna mipango gani ya kuweka mazingira wezeshi ya kupata mbegu bora za malisho kama Luseni pamoja na kuwezesha uzalishaji wa mitamba?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi; Serikali ina mpango gani wa kuimarisha Shamba la Mifugo la Kitulo wilaya ya Makete na shamba la mifugo la Sao Hill Iringa?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 tumedhamiria kuhakikisha kwamba tunaimarisha mashamba yetu matano likiwemo hili la Kitulo na lile la Mabuki na Sao Hill ambayo tutayaongezea zana za kazi kama vile matrekta na zana zile za kuweza kuvunia majani kwa maana ya malisho, lakini pia vilevile kwa kuyaongezea ng’ombe wazazi bora ili tuweze kuzalisha zaidi ya ng’ombe 3,500 na kuwasambaza nchini kote, kwa hivyo, mpango huu tunao na tunaelekea katika kuutekeleza, ahsante sana. (Makofi)