Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 33 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 292 2022-05-30

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya polisi katika Mahakama za Kata nchini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuwa na vituo vya polisi kila kata na ndio maana imeanzisha utaratibu wa Polisi Kata inayoongozwa na Mkaguzi wa Polisi. Ujenzi wa vituo hivyo utaendelea kufanyika kwa awamu kutegemea upatikanaji wa fedha. Vituo hivyo hutumiwa na mahakama zilizoko kwenye kata husika pindi vinapohitajika, nashukuru.