Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya polisi katika Mahakama za Kata nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali sasa nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza; swali la kwanza, kwa kuwa katika Mahakama ya Tarafa iliyopo pale Kiponzelo ilishatokea miaka ya nyuma hapo kwamba wakati mtuhumiwa anasafirishwa kwenda Ifunda alitoroka na kuonesha kwamba kulikuwa hakuna usalama.

Je ni lini sasa Serikali itaanza angalau kujenga vituo hivi vya polisi kwenye maeneo ya Tarafa hasa pale Kiponzelo?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili Ifunda tuna Kituo cha Polisi kikubwa bahati mbaya hatuna gari wala nyumba za polisi; je, ni nili Serikali sasa itaturekebishia angalau kupata gari hapo Ifunda? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kiswaga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu mfungwa aliyetoroka kwasababu ya umbali kama nilivyosema katika nyakati tofauti ninapojibu maswali haya kadri tutakapopata fedha tutajenga vituo vya polisi viwe karibu kabisa na maeneo ambayo yanahitajika ikiwemo karibu na Mahakama zilizopo ngazi ya Tarafa na ninajua pia mpango wa Serikali upande wa Wizara ya Katiba na Sheria ni kuweka Mahakama hizi katika kila Kata. Kwa hiyo niendelee kusisitiza wadau mbalimbali wakiwemo Serikali za Mitaa wadau kama yeye Mheshimiwa Kiswaga mwenyewe ana mpango wa kusaidia kujenga kituo cha polisi, vituo hivi vitakapojengwa tutapeleka askari.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu swali la pili kwamba kuna kituo lakini hakina gari wala nyumba nimeeleza mara kadhaa hapa kulingana na bajeti yetu ya mwaka huu na mkataba tulionao na kampuni ya Ashok Leyand tunayo magari ambayo tutapokea 78 mwezi huu, lakini vilevile hayo magari 78 yameshapokelewa ni taratibu za kuyatoa bandarini lakini mpaka mwezi Septemba tutakuwa tumekamilisha magari 396. Maeneo yenye changamoto kama haya ya Kalenga yatazingatiwa, nashukuru sana. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya polisi katika Mahakama za Kata nchini?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niipongeze Serikali kwa kusikia kilio change cha ujenzi wa Mahakama ya Wilaya katika Wilaya ya Nyang’hwale swali. Ni lini Serikali Itaanza ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Nyang’hwale?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amar kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa gereza la Nyang’hwale kama lilivyoombwa na Mheshimiwa Amar utaanza baada ya kuwa tumepata fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo, kwa kweli kwa mwaka ujao hatuna bajeti hiyo, lakini tutaingiza kwenye kipaumbele kutokana na mahitaji ya Wilaya ya Nyang’hwale, nashukuru. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya polisi katika Mahakama za Kata nchini?

Supplementary Question 3

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, pamoja na furaha tuliyonayo wananchi kuhusu mambo yaliyotokea Jumamosi huko Mwanza naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. (Makofi)

Wakati wenzetu wanang’ang’ania vituo vya Kata vya Tarafa Wilaya ya Kilombero ina Kata 35 na haina Kituo cha Polisi cha Wilaya; je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kilombero?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asenga, Mbunge wa Kilombero kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tumeshazungumza na Mbunge hiyo changamoto yake ya kituo, lakini tumesema katika maeneo yatakayopewa kipaumbele katika miaka ijayo tukianza na mwaka wa fedha 2022/2023 ni maeneo ya Wilaya ambayo hayana kabisa Vituo vya Polisi. Kwa hiyo matarajio yangu ndani ya mwaka mmoja miwili ijayo tutakuwa tumeanza ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kilombero kama ilivyoombwa na Mheshimiwa Mbunge.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya polisi katika Mahakama za Kata nchini?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa Mji wa Bashnet ambao ni Makao Makuu ya Tarafa hauna kituo cha polisi na badala yake polisi hutoka Mji wa Babati ambao ni kilometa 60 na kurudi jioni.

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Mji wa Bashnet ambao ni Makao Makuu ya Tarafa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Baran Sillo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunatambua baadhi ya maeneo kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge ana uhaba wa vituo umbali wa kilometa 60 ni umbali mkubwa na haukubaliki. Naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaweka kipaumbele kwenye eneo lake ili kuweza kuanza ujenzi wa Kituo hicho cha Polisi, nashukuru.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya polisi katika Mahakama za Kata nchini?

Supplementary Question 5

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na mimi kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza kwa Wizara ya Mambo ya Ndani.

Mheshimiwa Waziri mwaka 2017 mimi kama Mbunge na mwananchi wa Kata ya Mpona tulichanga fedha tukaanza kujenga Kituo cha Polisi kata ya mpona na angalau kwa asilimia 80 kimekamilika bado asilimia 20; je, Serikali haioni haja ya kuniongezea fedha kwa ajili ya kufanya finishing ya kituo hicho? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza tunawapongeza wananchi waliojitokeza na Mbunge wao kujenga kwa asilimia 80 kituo hicho na kuahidi kulipa kipaumbele. Nitamwelekeza IGP katika fungu lake la tuzo na tozo aweze kuweka kipaumbele katika eneo hili ili kuweza kukikamilisha kituo hicho. (Makofi)