Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 33 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 293 2022-05-30

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Handeni Kibirashi, Kondoa hadi Singida kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Handeni – Kiberashi – Kibaya – Chemba – Farkwa – Kwa Mtoro hadi Kititimo Singida kwa awamu ambapo mkataba wa mkandarasi wa kujenga sehemu ya Handeni – Mafuleta kilometa 20 ulisainiwa tarehe 11 Aprili, 2022. Ahsante.