Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Handeni Kibirashi, Kondoa hadi Singida kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. REUBEN N. KWAGILWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kwenye swali hili.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; ni lini sasa Serikali itamkabidhi mkandarasi huyu site ili ujenzi uweze kuanza mara moja? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili la nyongeza; barabara ya Handeni – Mziha – Turiani ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwa miaka karibia 30.

Je, Serikali haioni kwamba inakikosea Chama cha Mapinduzi kwa kutotekeleza ahadi yake ambayo ipo kwenye Ilani kwa miaka 30 iliyopita? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara hii kama nilivyosema kwenye jibu la msingi mkandarasi ameshasaini tangu tarehe 11 Aprili na anaitwa Hernan Highway Engineering Group Company Limited na sasa hivi anachofanya ni maandalizi kwa ajili ya kuanza ujenzi. Kwa hiyo, taratibu zitakapokamilika ili akamilishe site tutamkabidhi na tutapenda kwa kweli Mheshimiwa Mbunge aweze kuwepo wakati sasa anaanza kazi rasmi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu barabara ya Magole – Mziha – Handeni; Serikali imeeshaanza kwa kipande cha Magole – Turiani na katika mwaka huu wa fedha, fedha imetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara hii ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi lakini pia kuhakikisha kwamba hii barabara tunaijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Handeni Kibirashi, Kondoa hadi Singida kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Masasi – Nachingwea kuelekea Liwale kwa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Pathan, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Lindi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Masasi – Nachingwea kwenda Liwale Serikali imetenga bajeti kwenye bajeti ambayo imepitishwa kuanza na eneo la Masasi kwenda Nachingwea. Kwa hiyo, barabara hiyo tuna hakika itaanza utekelezaji kwa kiwango cha lami kwa mwaka fedha tunaoenda kuuanza sasa. Ahsante.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Handeni Kibirashi, Kondoa hadi Singida kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na mimi kupata nafasi.

Nilitaka kujua ni lini Serikali itatafuta fedha kwaajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Amkeni – Kitangali kwenda Mtama? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Mtanda, Mbunge wa Newala Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ina azma ya kujenga barabara zote kwa kiwango cha lami lakini kinachotegemea ni upatikanaji wa fedha na bajeti itakavyoruhusu. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kadri fedha itakavyopatikana barabara hii pia itaingizwa kwenye mpango ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Handeni Kibirashi, Kondoa hadi Singida kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya kutoka Kilosa – Ulaya kwenda Mikumi ambayo inapitia Masanze - Zombo na Ulaya ni barabara muhimu sana kwa kuchukua watalii kutoka SGR Station pale Kilosa kuja Mikumi mbugani na barabara hii ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010, 2015 na 2020.

Sasa kwa kuwa mimi siwezi kuruka sarakasi, nifanye nini ili Serikali ijue kwamba barabara hii ni muhimu kutengenezwa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Londo, Mbunge wa Mikumi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba barabara hii ilishaanza kujengwa ila bado haijakamilika nani azma ya Serikali kuikamilisha barabara hii na ni barabara ambayo inaunganishwa na barabara ya Mikumi – Kidatu hadi kwenda Songea.

Kwa hiyo, katika mipango ambayo Serikali inaendelea nayo kama alivyowasilisha Mheshimiwa Waziri wakati wa bajeti barabara ambazo zinafikiriwa pengine kujengwa kwa mpango wa EPC ili kuikamilisha barabara yote. Ahsante.