Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 34 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 294 2022-05-31

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya afya katika Jimbo la Lupembe ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Jimbo la Lupembe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka na imekwishaanza kutekeleza mpango wa kujenga vituo vya huduma za afya katika Jimbo la Lupembe.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilitenga shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya afya katika Jimbo la Lupembe. Aidha, hadi kufikia tarehe 30 Mei, 2022 imekwishapeleka shilingi bilioni 1.5 ambapo shilingi milioni 550 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya vya Ikondo na Kitiwa; shilingi milioni 150 kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati tatu za Ihang’ana, Maduma na Lyalalo; na shilingi milioni 800 kwa ajili ukarabati wa miundombinu ya Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Ahsante.