Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya afya katika Jimbo la Lupembe ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2021 Waziri wa TAMISEMI aliahidi kujenga kituo cha afya katika Kata ya Ikuna; je, Serikali ni lini itatimiza ahadi hiyo? Swali la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika Wilaya ya Kilolo, Kata ya Ukumbi, wananchi wamejenga jingo la kituo cha afya kwa nguvu zao wenyewe na OPD imekamilika; je, Serikali iko tayari kuelekeza fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika Kata ya Ukumbi ili majengo yale ya vituo vya afya yaweze kukamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nyamoga, Mbunge wa Kilolo kwa niaba ya Mheshimiwa Enosy Swalle Mbunge wa Lupembe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali tunatambua tuna commitment ya kupeleka fedha kujenga kituo cha afya cha Kata ya Ikuna, na Mheshimiwa Mbunge wa Lupembe, Mheshimiwa Edwin Swalle, amekuwa akifuatilia mara kwa mara kwa bidii sana kuhusiana na miradi ya maendeleo kwa ujumla, lakini Kituo cha Afya cha Ikuna. Nimhakikishie kwamba Serikali tayari tunatafuta fedha kwa ajili ya kwenda kujenga Kituo cha Afya cha Ikuna.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana na Kituo cha Afya cha Kilolo ambacho wananchi wamejenga niwapongeze sana wananchi wa Kilolo kwa kutoa nguvu zao na niwahakikishie kwamba Serikali imeweka mpango wa kuchangia nguvu za wananchi kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya na tutafanya hivyo, ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya afya katika Jimbo la Lupembe ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwa kuwa wananchi wa Kata ya Ihanda na Msia, wametenga maeneo na wametayarisha matofali na mawe kwa ajili ya vituo vya afya.

Je, upi mkakati wa Serikali katika kuwaunga wananchi hao kuhakikisha vituo vya afya hivyo vinajengwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hasunga Mbunge wa Jimbo la Vwawa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka mpango, kwa mwaka ujao wa fedha wa kukamilisha vituo vya afya, zahanati na hospitali za halmashauri, lakini kununua vifaa tiba kwa ajili ya kuhakikisha vituo vile vinaanza kutoa huduma na baada ya hapo sasa tuaendelea na ukamilishaji wa vituo vya afya, vikiwemo vituo vya afya vya Jimbo la Vwawa.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya afya katika Jimbo la Lupembe ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali, je ni lini Serikali itaanza ukarabati wa Kituo cha Afya cha Mwika, kwa kuongeza jingo la wodi ya watoto pamoja na jengo la upasuaji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Charles Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Kimei, amefuatilia sana suala la ukarabati wa Kituo cha Afya cha Mwika, na sisi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, tulishamhakikishia kwamba tunatafuta fedha kwa ajili ya kujenga wodi ya watoto, wodi ya upasuaji lakini pamoja na ukarabati wa kituo kile na tutafanya hivyo.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya afya katika Jimbo la Lupembe ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nataka kujua Kituo cha Afya Honyali, tulikipelekea shilingi milioni 250 wajenge na baada ya hapo wataongeza milioni 250 kukimalizia. Wananchi wamejitahidi kwa kupitia Halmashauri ya Bunda na wako katika hatua nzuri. Ni lini sasa hela ya pili itaenda shilingi milioni 250 ili wamalizie kituo chao?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tulipeleka shilingi milioni 250 na kazi ya Ujenzi wa Kituo cha Afya inakwenda lakini masharti ni kwamba baada ya kukamilisha ujenzi wa shilingi milioni 250 ndipo shilingi milioni 250 nyingine zitapelekwa. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba tutapeleka mara baada ya kukamilisha matumizi ya shilingi milioni 250 ya kwanza. Ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya afya katika Jimbo la Lupembe ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi?

Supplementary Question 5

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia zaidi ya halmashauri tano na pia iko kando kando ya barabara kuu ya kwenda Zambia mpaka South Africa. Kutokana na sababu hiyo imekuwa na msongamano mkubwa sana wa wagonjwa katika kutoa huduma.

Je, Serikali iko tayari kupitia basket fund, kuongeza bajeti katika Hospitali hii ya Mafinga ambayo inahudumia halmashauri zaidi ya tano?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Hospitali ya Mji wa Mafinga iko barabara inahudumia wananchi wengi kutoka pia kwenye kata na halmashauri za jirani, na utaratibu wa fedha za basket fund utaendelea kutolewa kulingana na population iliyoko ndani ya halmashauri husika na ndicho kinachofanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la msingi nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi sasa Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan inajenga vituo vya afya katika kata zote za kimkakati na hospitali za halmashauri katika halmashauri ambazo hazina hospitali. Kwa hiyo, automatically tutapunguza wagonjwa ambao wengi wanakwenda hospitali ya Mji wa Mafinga.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya afya katika Jimbo la Lupembe ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi?

Supplementary Question 6

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Ninatambua mchango wa Mbunge wa Jimbo la Rungwe katika kuchangia Zahanati ya Kiwira, Serikali mtatuongezea lini fedha ili aweze kumalizia jengo hilo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kwamba wananchi wamechangia nguvu zao na kujenga Zahanati ya Kiwira na nimhakikishie Serikali imeweka mkakati ambao kwa awamu kadri ya upatikanaji wa fedha tunafanya tathmini na kuongezea fedha na kukamilisha majengo hayo na tunafanya pia tathmini katika Zahanti hii ya Kiwira. Ahsante.