Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 34 Water and Irrigation Wizara ya Maji 297 2022-05-31

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MH. TASKA R. MBOGO aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Katavi wanapata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Katavi ni wastani wa asilimia 71 kwa vijijini na asilimia 60 kwa mijini. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji 42 katika Wilaya zote za Mkoa wa Katavi lengo likiwa ni kuhakikisha Wananchi wanapata maji safi na salama. Miradi hii ni pamoja na mradi wa maji Karema kwa kutumia Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Tanganyika unaotarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2022. Vilevile Mji wa Mpanda utanufaika na utekelezaji wa mradi wa maji wa miji 28.

Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itaajiri Mtaalamu Mshauri wa kufanya usanifu kwa kutumia vyanzo vya Ziwa Tanganyika ili kuwapatia maji wananchi wa Wilaya za Tanganyika, Mlele, Mpanda na maeneo ya karibu na kufikia lengo la asilimia 95 mijini na asilimia 85 vijijini ifikapo mwaka 2025.