Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MH. TASKA R. MBOGO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Katavi wanapata maji safi na salama?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, wananchi wa Mkoa wa Katavi hususani Wilaya ya Mpanda Kata za Majengo, Kashaulili, Mpanda Hotel wamekuwa na mgao wa maji hawapati maji kila siku, lakini lipo Bwana la Milala ambalo lilikuwa ni chanzo cha maji sasa hivi bwawa hilo halitumiki kwa sababu limechafuka. Je, Serikali ina mkakati gani wa kusafisha bwawa hilo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Ziwa Tanganyika ndiyo chanzo kikuu cha kutoa matatizo ya maji kwenye Mkoa wa Katavi; Serikali ina mkakati gani wa kuharakisha upembuzi yakinifu ili maji yaweze kutoka Ziwa Tanganyika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Mbogo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, awali yayote napokea pongezi, lakini vilevile napenda kurudi kwenye jibu langu la msingi eneo la Mpanda linakwenda kunufaika hivi punde na ule mradi wetu mzuri ambao tumeusubiri kwa muda mrefu na Mheshimiwa Rais hivi punde anakwenda kufanya yake na maji yanakwenda kuanza kutekelezwa kupitia mradi wa miji 28.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na bwawa kuchafuka, tutaangalia uwezekano wataalamu watakwenda kuangalia uwezekano wa kuona kama bwawa hili litatufaa au litatupotezea fedha, kama litakuwa linahitaji fedha nyingi ambayo haina tija sana kwenye matokeo tutaendelea na mikakati mingine, lakini suala la msingi ni kuhakikisha wananchi wanakwenda kupata maji safi na salama bombani.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la matumizi ya Ziwa Tanganyika ni moja ya mikakati ya wizara nimekuwa jibu hili mara kadhaa tutakwenda kutumia Ziwa Tanganyika kwasababu hakuna asiyefahamu kwamba ni chanzo ambacho kitatuletea tija kubwa sana na miradi itabaki kuwa endelevu kwa vizazi na vizazi.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MH. TASKA R. MBOGO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Katavi wanapata maji safi na salama?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na kilio kikubwa sana kwa wakazi wa Mkoa wa Simiyu hususani Wilaya za Busega, Itilima na Meatu; je, ni lini akina mama wa mkoa huo watafaidika na maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Minza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Simiyu unakwenda kunufaika na mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria mradi ambao ni mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira na tunatarajia maeneo hayo yote aliyoyataja yanakwenda kunufaika, Meatu ipo katika mpango huo na tayari wananchi wameanza kulipwa fidia. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MH. TASKA R. MBOGO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Katavi wanapata maji safi na salama?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwanza niipongeze Serikali na Wizara yake ya Maji kwa kuzidi kutukamilishia mradi wetu wa maji na maji yameshaingia maeneo mbalimbali katika Wilaya ya Nyang’hwale, lakini wananchi wanalalamika bei ya maji ni kubwa ukilinganisha na mjini. Nyang’hwale tunalipa shilingi 2500 kwa unit moja wakati Mji wa Geita na Mwanza wanalipa 1,350.

Je ni lini Serikali itatoa kauli kwa Wilaya ya Nyang’hwale kupunguza bei ya maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amar, Mbunge wa Nyang’hwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya Nyang’hwale pamoja na maeneo mengine kama Karatu tunafahamu bei bado si rafiki sana kwa wananchi na hii ilisababishwa na utekelezaji wa mradi, lakini kama Wizara tunaendelea kufanya mapitio ili kuona kwamba bei zinakwenda kuwa bei rafiki kwa wananchi. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MH. TASKA R. MBOGO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Katavi wanapata maji safi na salama?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru; mradi wa maji wa Nansio Jimboni Ukerewe ulishakamilika na kuanza kutoa huduma, lakini bado maji hayajaweza kuwafikia wananchi wote zinahitajika bomba takribani kilometa kama 67 ili kuweza ku-cover eneo lote na maji yawafikie wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipo tayari sasa kusaidia mamlaka hii ya maji bomba hizi ili huduma ya maji iweze kuwafikia wananchi wote kwenye Mji wa Nansio? Nashukuru.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaposema mradi umekamilika tunahitaji kuona maji bombani, hivyo kama tumeshakamilisha mradi wa fedha nyingi hili suala la usambaji wa mabomba kuwafikia wananchi ndiyo jukumu letu kubwa. Hivyo nipende kukutoa hofu Mheshimiwa Mbunge tutafika na tutafanya kwa pamoja na wananchi wanakwenda kunufaika na maji bombani.