Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 34 Water and Irrigation Wizara ya Maji 298 2022-05-31

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatua ndoo kichwani wanawake wa Mji wa Mlowo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ni kuhakikisha huduma ya upatikanaji wa maji inaboreshwa nchi nzima. Hali ya upatikanaji wa maji katika Mji wa Mlowo ni wastani wa asilimia 44.5. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imekamilisha mradi wa maji wa Selewa - Mlowo ambapo mradi wa maji wa Mahenje - Mlowo utakamilika mwezi Juni, 2022. Miradi hii itaboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwa asilimia 53.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itatekeleza mradi kwa kutumia chanzo cha maji cha Mto Bupigu ulioko Wilayani Ileje. Aidha, mpango wa muda mrefu ni kujenga miundombinu ya kuchukua maji kutoka mradi mkubwa wa Mto Kiwira ambao utahudumia Jiji la Mbeya na maeneo jirani ikiwemo Mji wa Mlowo na maeneo ya pembezoni.