Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatua ndoo kichwani wanawake wa Mji wa Mlowo?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, kwa kuwa nimekuwa nikifuatilia mradi huu kwa muda mrefu sana na majibu ya Serikali yamebaki kuwa haya haya.

Sasa naomba kupata commitment ya Serikali inawahakikishiaje wanawake wa Mlowo, wanawake wa Vwawa na Tunduma kwamba ni kweli kwa mwaka wa fedha ujao watatuletea mradi huu wa kutoa maji Ileje na kuweza kuyasambaza kwenye maeneo hayo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Serikali imekiri kwamba hatuwezi kumaliza tatizo la maji kwa kujenga miradi midogo midogo; sasa naomba kufahamu tunaye mkandarasi ambaye anatatujengea miradi ya maji katika Kata ya Mkwajuni pamoja na Galula kule Songwe, lakini mpaka sasa hivi hajamaliziwa fedha na huo mradi umeanza mwaka 2019.

Je, ni lini sasa Serikali itammalizia fedha mkandarasi huyo ili kuweza kuwapunguzia adha ya maji wanawake wa Wilaya ya Songwe? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shonza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, commitment ya Serikali ni kuhakikisha maji yanapatikana maeneo yote nchini na hili tumeona jitihada za dhati kabisa Mheshimiwa Rais ametoa fedha nyingi zaidi ya asilimia 95 mpaka sasa, mpaka tumalize mwaka huu wa fedha itakuwa zaidi ya hapo. Hivyo, Serikali tutafika maeneo yote na kuhakikisha miradi ambayo haikutekelezeka inakwenda kutekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na mkandarasi kulipwa Mkwajuni – Songwe wakandarasi wanaendelea kulipwa kulingana na walivyofanyakazi walivyo raise certificates na kuna sababu mbalimbali zinazopelekea hawa baadhi ya wakandarasi malipo yao kuchelewa hivyo niwatake wakandarasi wote wafanyekazi kadri ya mikataba nakwa ambaye hajalipwa basi aweze kufuata taratibu ili malipo yake yaweze kufanyika mara moja.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatua ndoo kichwani wanawake wa Mji wa Mlowo?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Waziri mwaka jana wakati akijibu swali langu la msingi kwenye swali la nyongeza aliniahidi kunipatia fedha kwa ajili ya kuchimba kisima kimoja cha maji katika Kijiji cha Nainokwe.

Je, lini fedha hizi zitakwenda ili wana Nainokwe wakafarijike kutokana na adha ya maji wanayoipata?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifika tulifanya pamoja ziara na kisima hiki ni lazima kichimbwe. Mheshimiwa Mbunge tafadhali baada ya session hii ya leo tukutane ili tuweze kufuatilia pamoja hii fedha itoke. (Makofi)

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatua ndoo kichwani wanawake wa Mji wa Mlowo?

Supplementary Question 3

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru; Tarafa ya Murongo imepatakana na Mto Kagera ambako ni chanzo kikubwa cha maji, lakini hizo kata hazina maji.

Nataka kujua nini mkakati wa Serikali katika kuwatua kina mama ndoo kusaidia upatikanaji Kata ya Kibingo, Bugomora, Murongo, Kibale, Kimuli, Bugara na Businde? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tarafa hiyo ya Murongo aliyoitajwa ni moja ya maeneo tunaendelea kuyafanyikazi na kwasababu ipo karibu na chanzo cha uhakika naomba nitoe wito kwa wananchi tuendelee kuvumilia, tunakotoka ni mbali tunakokwenda ni karibu, hizi kata zote zinakwenda kupata huduma ya maji na salama.