Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 34 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 300 2022-05-31

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Igunga?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI, alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nicholaus George Ngassa, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Gereza la Igunga lilianza kujengwa mwaka 2004 na lilifunguliwa rasmi mwaka 2006. Hadi sasa mabweni mawili ya wanaume yenye uwezo wa kulala wafungwa 51 kila moja yamekamilika na ujenzi wa jengo la utawala sambamba na nyumba za askari unaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, juhudi za kukamilisha ujenzi wa Gereza hili zinaendelea na fedha kiasi cha shilingi 77,694,000 zimetengwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya umaliziaji wa jengo la utawala. Nashukuru.