Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana; cha kwanza nataka nimwambie Mheshimiwa Naibu Waziri anavyosema kwamba mabweni mawili yamekamilika si kweli kwa sababu yale mabweni hayajakamilika. Mpaka sasa wameziba kwa mabanzi na mbao chakavu kwa ajili ya kuwa-accommodate wale wafungwa, jambo ambalo ni kinyume cha haki za binadamu na utawala bora. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wake walifanyie kazi waweze kulikamilisha gereza hili ili liweze kutoa huduma vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili,, kwa sasa Serikali inapata hasara kwa kuwa mabweni ya wanawake hayapo, inasababisha kama kuna mfungwa ambaye ana kesi mbili au kesi inaendelea anachukuliwa anatolewa Igunga anapelekwa Nzega na inapoitwa kesi mahakamani inabidi arudishwe. Jambo ambalo linaingiza Serikari hasara.

Je, haoni kuendelea kuingiza Serikali hasara wasipomaliza ujenzi wa hili gereza? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ngassa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza hili ambalo ameniambia kwamba majengo hayajakamilika na ni machakavu kwangu pia ni jipya. Nachukua dhima ya kuongozana na wataalam wetu baada ya Bunge hili kwenda Igunga kujiridhisha, kuona ukweli wa hiki ambacho kinasemwa na kwa kweli kama tutakuwa iko tofauti tutachukua hatua stahiki kwa hawa waliotupa majibu haya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la mabweni ya wanawake kutokuwepo Igunga tunatambua, lakini kama nilivyokwishasema tunajenga kulingana na upatikanaji wa bajeti. Kwa vile hatujapata fedha akubali tu Mheshimiwa hawa wafungwa wa kike waendelee kupelekwa katika gereza la jirani. Lakini mipango ya Wizara ni kuendelea kujenga mabweni hitajika, na kwa sababu angalau mwaka huu tuna bajeti tuweze kuona jinsi ambavyo tutaweza kuwa-accommodate akinamama ambao wanakuwa wanasafirishwa kwenda gereza la mbali. Nashukuru.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na samahani sauti yangu imekuwa mbaya leo.

Kwa kuwa kuona ni kuamini, je, Mheshimiwa Naibu Waziri ni lini tutafuatana mimi na wewe kwenda Kingurungundwa ambako kuna gereza la miaka mingi na gereza hili ni la mabati na hali yake ni mbaya sana? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Kikwete kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana naye kuona ni kuamini na niko tayari kuongozana naye wakati wowote baada ya shughuli za Bunge ili pamoja na mambo mengine kuangalia uchakavu wa gereza hili. (Makofi)

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 3

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa gereza la Wilaya ya Manyoni limejengwa miaka 52 iliyopita hali inayopelekea miundombinu yake kuwa ni chakavu sana. Je, ni lini Serikali itakarabati na kufanya upanuzi wa gereza hili ili kupunguza msongamano katika gereza hili? Nakushukuru.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aysharose Mattembe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakubali baadhi ya magereza ikiwemo la Manyoni ni la muda mrefu na lina uchakavu na ndiyo maana tumeanza mkakati wa kukarabati magereza chakavu kama tulivyokwishafanya Liwale na maeneo mengine. Nachukua ahadi kwamba tutaendelea kukarabati magereza haya kulingana na upatikanaji wa fedha. Nashukuru.