Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 34 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 301 2022-05-31

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:-

Je, nani anahusika kukamilisha ujenzi wa viwanja vya michezo Nelson Mandela University ili shughuli za michezo ziendelee?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa viwanja vya michezo katika Taasisi ya Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia umefanywa na Mkandarasi Elerai Construction Company Ltd. chini ya usimamizi wa Chuo Kikuu cha Ardhi. Hata hivyo, wakati ujenzi unaendelea kulijitokeza dosari na hivyo ujenzi haukukamilika na kusimama.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu ndiyo inayohusika na ukamilishaji wa ujenzi huo. Hivyo mwezi Machi, 2021 Wizara iliitisha kikao cha wahusika wote wa mradi huo ambao ni Wizara ya Fedha na Mipango, Pension Property Ltd., Taasisi ya Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia, Mshauri Elekezi na Mkandarasi kujadili suala hili. Katika kikao hicho ilikubalika kuwa Chuo Kikuu cha Ardhi kiendelee kumsimamia mkandarasi Elerai na kuhakikisha anakamilisha kazi ya ujenzi wa viwanja hivyo. Nakushukuru sana.