Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:- Je, nani anahusika kukamilisha ujenzi wa viwanja vya michezo Nelson Mandela University ili shughuli za michezo ziendelee?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la ujenzi wa kiwanja hicho umechukua miaka saba, kama kuna hilo tatizo, sijui mgogoro inanishangaza.

Je, Serikali sasa ina mpango gani wa ku-review mkataba huo ili kuhakikisha ujenzi huo unakamilika na kiwanja kinatumika mara moja? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wa karibu wa suala hili. Kabla hajaliuliza hapa bahati nzuri aliwahi kufika ofisini na tulilijadili kwa kina.

Nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge katika kikao hiki cha tarehe 4 Machi, 2021 pamoja na mambo mengine kilijadili vilevile kufanya review ya mkataba lakini vilevile kufanya review ya design ya viwanja vile. Kwa hiyo, nimuondoe wasiwasi, review imeshafanyika na mchakato sasa mwingine unaendelea katika kuhakikisha kwamba tunafanya review ya thamani au gharama za ujenzi ili kazi hii iweze kukamilika kwa haraka. Nakushukuru sana.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:- Je, nani anahusika kukamilisha ujenzi wa viwanja vya michezo Nelson Mandela University ili shughuli za michezo ziendelee?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, baadhi ya vyuo nchini vinakabiliwa na ukosefu wa viwanja vya michezo.

Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka Wizara kupita kwenye Wilaya zote na Mikoa kuona viwanja vilivyopo na namna ya kushirikiana na wadau? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Issaay kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tukakubali kwamba kuna changamoto ya viwanja kwenye maeneo yetu ya vyuo, tunaomba tubebe/tuchukue ushauri huu wa Mheshimiwa Issaay ili tuweze kwenda kufanya tathmini namna gani tunaweza kushirikiana na wadau wengine kuweka kufanya maendeleo ya viwanja kwenye vyuo vyetu. Nakushukuru sana.