Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 34 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 302 2022-05-31

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali juu ya kuvuja kwa mitihani inayosimamiwa na vyuo vya afya mwaka 2021?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inakiri kutokea kwa changamoto ya kuvuja kwa mitihani inayosimamiwa na vyuo vya afya mwezi Agosti, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imechukua hatua zifuatazo ili kuhakikisha kuwa tatizo hili halijitokezi tena kwa kufanya mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza; ni kuboresha mfumo wa utungaji, uchapishaji na ufungaji wa mitihani kwa kushirikiana na Mpiga Chapa wa Serikali.

Jambo la pili ni kufanya mapitio ya Mwongozo wa Mitihani iliyo chini ya Wizara ya Afya ili kuendana na mahitaji ya kiulinzi na kiusalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu ni kuongeza kasi ya kuanzishwa Mamlaka itakayosimamia mafunzo ya vyuo vya afya ngazi ya kati pamoja na uendeshaji wa mitihani.

Jambo la nne ni kushirikisha vyombo vya ulinzi na usalama kwenye ulinzi wa mitihani katika hatua zote kuanzia utungaji, usambazaji hadi utoaji wa matokeo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.