Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali juu ya kuvuja kwa mitihani inayosimamiwa na vyuo vya afya mwaka 2021?

Supplementary Question 1

MHE PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili ni nyeti sana, mimi ni mtu wa elimu. Suala hili limeulizwa leo ni mara ya pili; mimi kama mlezi wa TAMOSCO, elimu upande wa vyuo na elimu msingi na sekondari napata shida sana pale ambapo kwenye shule za msingi, kwenye shule za sekondari O-level na A-level mitihani ikivuja na hasa kwenye shule za private Serikali inachukua hatua haraka na kuwapeleka mahakamani na kuwapa adhabu na ikiwezekana kufunga shule.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala hili limejitokeza Wizara ya Afya kwa NACTE ambao ni watu wa Serikali, liko kimya, ni kimya kimya wanafunzi wamerudia mitihani, wameenda wamefanya kimya kimya na wazazi wamepata adha ya kurudia mtihani na kulipia zile ada mara ya pili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nini kauli ya Serikali kuwapa adhabu Maafisa wote wa Serikali Wizara ya Afya waliohusika na uvujaji wa mitihani? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa hoja yake muhimu ambayo mara nyingi sana na yeye huwaga tunashirikiana na anakuja ofisini mara nyingi. Mheshimiwa Mbunge nikutoe wasiwasi, tunakwenda kuhakikisha kwamba maeneo haya tunakwenda kuyasimamia vizuri kwa mujibu wa kanuni, sheria, taratibu na miongozo iliyopo. Na nikuondoe wasiwasi kwamba jambo lile tayari limeshachukuliwa hatua na liko kwenye hatua za mwisho kabisa kuhakikisha kwamba adhabu inatolewa kwa wale wote waliohusika kwenye jambo hili. Nakushukuru sana.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali juu ya kuvuja kwa mitihani inayosimamiwa na vyuo vya afya mwaka 2021?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana. Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba mitihani hii imevuja na inasimamiwa na Wizara ya Afya. Nataka kujua wajibu wa NACTE katika kusimamia mitihani hii ni nini? Ahsante sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Sima kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, wajibu wa NACTE kwenye uratibu wa zoezi zima la mafunzo katika vyuo vyetu vyetu vya kati ni pamoja na mitihani hii. Lakini kwa upande wa mitihani ile ya muhula wa kwanza, mara nyingi sana inafanyika na kusimamiwa na kuratibiwa na Wizara ya Afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimezungumza kwenye majibu yangu ya msingi kwamba tunakwenda kuanzisha chombo maalum kitakachokuwa kinaratibu masuala haya ya mitihani katika Wizara ya Afya kwa ujumla wake ambayo itashirikiana sasa na NACTE kwa ukaribu. Kwa hiyo, matatizo haya tunakwenda kuyamaliza na kuyaondoa kabisa. Nakushukuru. (Makofi)