Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 35 Water and Irrigation Wizara ya Maji 312 2022-06-01

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:-

Je, ni lini Wananchi wa Kata ya Bosha na Mhinduro watapata maji salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Jimbo la Mkinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha usanifu wa Mradi wa Maji wa Mhinduro utakaohudumia Kata za Bosha na Mhinduro na ujenzi utaanza mwezi Juni, 2022 na kukamilika katika mwaka wa fedha 2022/2023.