Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Kata ya Bosha na Mhinduro watapata maji salama?

Supplementary Question 1

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pia naishukuru Serikali kwa majibu, naomba kuuliza swali moja tu la nyongeza. Taarifa nilizonazo ni kwamba, mpaka sasa mkataba wa mradi huu haujasainiwa na kwa muda uliobaki Waziri anatuhakikishia kwamba, tutaweza kusaini mkataba huo na ujenzi wa mradi huu uweze kuanza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dunstan Kitandula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ndio. Wizara tutaweza kusaini mkataba na kazi zitaanza.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Kata ya Bosha na Mhinduro watapata maji salama?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa muda mrefu sana Serikali iliahidi kupeleka maji katika Shule ya Nanja, Kijiji cha Mti Mmoja na Lepurko vilivyoko katika Wilaya ya Monduli, Mkoa wa Arusha, lakini hadi leo haijatimiza ahadi yake. Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi yake katika vijiji hivi, ili wanafunzi hawa na wananchi waepukane na adha hii kubwa ya maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuliahidi eneo la shule hii pamoja na hiki kijiji alichokitaja viweze kupatiwa huduma ya maji. Hatujapeleka kwa sababu ya mtawanyiko wa majukumu, lakini ni lazima tutapeleka maji katika shule hii na hiki kijiji na maeneo ya shule nyingine zote katika Jiji la Arusha, lakini vilevile na vijiji vyote.

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Kata ya Bosha na Mhinduro watapata maji salama?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii. Licha ya juhudi kubwa za Serikali za kutatua changamoto ya maji Mkoani Tanga, bado Wilaya ya Muheza inapata maji kwa mgawo tena saa 8.00 za usiku. Je, ni lini Serikali itawezesha maji yale kutoka mapema ili wanawake wa Muheza waweze kupumzika usiku?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Tanga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, eneo la Muheza kutoa maji ya mgawo usiku wa manane, huu sio utaratibu mzuri na tunataka kukomesha hili. Naomba wananchi wawe watulivu na subira, tutahakikisha huduma ya maji inapatikana saa zote na kama ni saa chache basi muda rafiki.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Kata ya Bosha na Mhinduro watapata maji salama?

Supplementary Question 4

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakabidhi Mradi ulioko katika Kata ya Vuje, Wilaya ya Same, ambao ulianza tangu 2018 ambao uligharimu takribani Sh.1,300,000,000?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, miradi ikishakamilika ni wajibu wa Wizara kukabidhi kwa wananchi na unaendeshwa na vile vikundi vidogo vidogo ambavyo vinaundwa na wananchi. Kwa hiyo na mradi huu ambao umeshatumia fedha ya Serikali zaidi ya bilioni ni lazima nao uje ukabidhiwe kwa wananchi, ili lengo la kufikisha huduma ya maji kwa wananchi liweze kutimia.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Kata ya Bosha na Mhinduro watapata maji salama?

Supplementary Question 5

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kuuliza swali moja la nyongeza. Je, ni lini mkandarasi wa kujenga Mradi wa Ngana Group atapatikana?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Mlaghila, Mbunge wa Kyela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Ngana Group taratibu ziko mwishoni. Tunatarajia kabla ya mwaka huu wa fedha kwisha, mkandarasi atapatikana na kazi ziweze kuendelea.