Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 39 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 346 2022-06-07

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya wananchi wa Kipunguni waliozuiwa kuendeleza maeneo yao kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Kamoli, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo katika hatua za mwisho za kufanya uthamini mpya kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi wote wa Kipunguni waliopisha ununuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA). Zoezi la uthamini linatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2022. Ahsante.